Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Serikali yamwaga ajira kwa Waalimu wa Sayansi na Hisabati

SERIKALI imetangaza kuajiri walimu wa masomo ya sayansi na hisabati katika shule za sekondari ambao wametakiwa kupeleka nakala za vyeti vyao vya elimu ya sekondari, vya taaluma ya ualimu (stashahada na shahada) kwa ajili ya uhakiki.

Tangazo kwa Umma lililotolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Maimuna Tarish lilisema vyeti vya sekondari vinavyotakiwa kuhakikiwa ni vya kidato cha sita.

Alisema ajira hizo ni kwa walimu wa Stashahada na Shahada za Mafunzo ya Ualimu wa Masomo ya Hisabati na Sayansi waliohitimu mwaka 2015.

Alisema nakala hizo ziwasilishwe kupitia barua pepe ya wizara kuanzia jana hadi Ijumaa ya Desemba 16 mwaka huu na yeyote ambaye vyeti vyake havitahakikiwa hatafikiriwa katika uajiri.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top