Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Mkulima amfungia safari Rais Magufuli

Mkulima wa tumbaku aliyesafiri kutoka Wilaya ya Urambo mkoani Tabora, Moshi Rubibi akitafuta upenyo wa kumfikishia Rais John Magufuli kilio cha wakulima, alifanikiwa kufanya hivyo mjini Bukoba  wa kutumia staili iliyomvuta Rais kumsikiliza.

Awali, mkulima huyo anayewakilisha wenzake zaidi ya 60 alikwama kufanya hivyo wakati Rais Magufuli alipokuwa kwenye mapumziko wilayani Chato mkoani Geita baada ya kuzuiwa na walinzi lakini bila kukata tamaa alimfuata Rais mjini Bukoba baada ya kusikia anafanya ziara.

Utaratibu wa Rais Magufuli kutaka kusalimiana na wananchi baada ya mkutano ndiyo uliofanikisha mpango wa mkulima huyo kwani aliamua kupiga kelele mfululizo kwa mbali akilitaja jina la Rais huku akipunga hewani mkono uliokuwa na bahasha ya kaki.

Pamoja na kudhibitiwa na walinzi, sauti ya mkulima huyo ilizidi kuchomoza kwa nguvu hali iliyomfanya Rais Magufuli aliyekuwa anaondoka kwenye eneo la mkutano kupiga hatua kadhaa nyuma na kuwaambia walinzi wake wamuache amsikilize.

Huku akitweta na kuhema kwa nguvu baada ya kuruhusiwa kumfikia Rais Magufuli, mkulima huyo alimwambia kuwa yeye ni mwenyeji wa Urambo, Tabora na amemtafuta ili kumfikishia malalamiko ya wakulima wa tumbaku wanaopigwa chenga kulipwa mafao yao.

Alisema wakulima hao wanadai zaidi ya dola za Marekani 98,000 (zaidi ya Sh200 milioni) za mauzo ya tumbaku waliyouza kupitia Bodi ya Tumbaku tangu Septemba, 2015 na kuwa wanashawishiwa kutoa rushwa ili wapewe haki yao.

Alimwambia Rais kuwa wameambiwa watoe dola 10,983 ili waweze kulipwa fedha zao kupitia tawi la Benki ya CRDB Urambo na kuwa kati ya kiwango wanachodai cha mauzo ya tumbaku wakubali kulipwa dola 87,017 tu.

Mkulima huyo alisema wamefikisha suala hilo kwa Mkuu wa Wilaya ya Urambo na kukosa ufumbuzi na kuwa walilipeleka pia kwa aliyekuwa Waziri wa Kilimo na Mifugo, Mwigulu Nchemba ambaye alionyesha kuwa tayari kulishughulikia lakini kabla ya kufanya hivyo, alihamishiwa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Baada ya kumsikiliza takribani kwa dakika nne, Rais Magufuli alimkabidhi mkulima huyo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu), Jenista Mhagama na kuagiza apewe taarifa baada ya siku tano jinsi walivyoshughulikia suala hilo.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top