Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Mwenyekiti Chadema na wenzake 7 wafikishwa mahakamani

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Wilaya ya Karatu mkoani Arusha, Thomas Darabe na wenzake saba wamepandishwa kizimbani kujibu shitaka la kuharibu mali ya thamani ya zaidi ya sh milioni 75.4 na vitunguu.

Pamoja na Darabe, waliopandishwa jana katika Mahakama ya Wilaya ya Arusha/ Arumeru ni Charles Lameck ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya watumia maji ya ya vijiji saba vilivyoko katika wilaya ya Karatu na George Pius.

Wengine ni Baridi John, Christopher Lameck, Florian Tiofil, Daniel Ninida na Lazaro Emmanuel.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya watumia maji alishitakiwa na mashitaka manne pekee yake ya thamani ya zaidi ya sh milioni 60 katika Mahakama ya Wilaya ya Arusha na Mahakama ya Wilaya ya Arumeru.

Akisomewa shitaka la kwanza na Mwendesha mashitaka wa serikali, Charles Gakirwa mbele ya Hakimu Mkazi Patricia Kisinda, alidai kuwa Desemba 28 mwaka huu mtuhumiwa alifanya uharibifu wa mali aina ya pampu ya maji ya thamani ya sh milioni tatu na bomba la maji la sh 448,000.

Shitaka la pili lililosomwa wakili wa serikali Gakirwa mbele ya hakimu mkazi wa wilaya ya Arusha , Devotha Msofe ilidaiwa kuwa Lameck alifanya uharibifu katika wa mfumo wa maji katika kijiji cha Quandet Karatu wa thamani ya zaidi ya sh milioni 1.6.

Mtuhumiwa alikana mashitaka yote na alipewa dhamana ya mtu mmoja na wadhamini wakifanikiwa kukidhi vigezo vyote katika mashitaka hayo. 

Katika mashitaka yaliyowahusu washitakiwa wote, akiwemo Darabe pamoja na Lameck ilidaiwa kuwa wote kwa pamoja walitenda kosa la uharibifu wa mali kwa kuchoma pampu ya maji ya thamani ya zaidi ya sh milioni tatu na injini ya maji ya thamani ya sh milioni 12.

Shitaka la tatu lililokuwa likiwakabili washitakiwa wote ni kuharibu mazao aina ya vitunguu ya thamani ya zaidi ya sh milioni 49 na pampu mbili za sh milioni sita. 

Washitakiwa wote walikana mashitaka hayo na dhamana zao zilikuwa wazi na upelelezi wa kesi hiyo ulikuwa bado haujakamilika na kesi hiyo itatajwa tena januari 16 mwaka huu.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top