Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein amemtaka mkuu wa mkoa wa Mjini Magharibi kuwatafuta na kumpelekea majina ya viongozi wanaosababisha migogoro ya ardhi katika mkoa huo haraka iwezekanavyo.
Agizo hilo amelitoa leo wakati akitamatisha ziara yake ya siku 3 iliyoanza juzi Ijumamosi mkoani humo, ambapo amesema moja ya mambo aliyokutana nayo ni pamoja matatizo ya ardhi ambayo yanasababishwa na viongozi wabadhirifu na kuagiza watafutwe na apatiwe majina yao ili ashughulike nao maramoja
Mbali na agizo hilo, Rais Shein pia amemuagiza Mkuu wa mkoa huo Ayoub Mohamed Mahamoud kushgulikia masuala kadhaa ikiwemo Wizi, Msongamano wa magari, Kutoa elimu ya usalama barabarani kwa watumiaji wote, kukumbusha tatizo la Ukimwi kuwa bado lipo, Usafi wa masoko, Gari zisiingie katikati ya mji mkongwe bila utaratibu.
Hata hivyo Rais Shein amefurahishwa na namna mkoa huo chini ya RC Ayoub Mohamed Mahamoud ulivyotekeleza miradi ya maendeleo kwa kasi kubwa.
Rais Shein alianza ziara yake siku ya Ijumamosi katika wilaya ya mjini, Siku ya Ijumapili alizuru wilaya ya Mjini magharibi 'A' na leo siku ya Ijumatatu amemalizia katika wilaya ya Magharibi 'B' mkoani humo ambapo alikagua na kuzindua miradi ya maendeleo.
Loading...
BLOG RAFIKI
-
-
-
-
-
Kurasa za Magazeti ya Leo Mei 02, 202415 hours ago
-
-
-
-
-
-
-
-
-
-
-
-
-
-
-
-
-
-
-
-
-
-
-
-
-
-
-
Post a Comment