Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

HUU NDIOUGONJWA HATARI WA EBOLA

 

Wagonjwa wa ebola wakipatiwa matibabu.
 
EBOLA ni ugonjwa unaosababishwa na virusi vya ‘ebola’ ambavyo hupatikana kwa wanyama wa porini hasa waishio katika maeneo yenye joto katika nchi za Afrika.
Jina la ugonjwa huo, yaani ebola, limetokana na Mto Ebola, uliopo nchini DR Congo.

AINA TANO ZA EBOLA

Zipo aina tano za virusi vya ugonjwa huu na majina yake yamepatikana kulingana na mazingira yake.
Kwa mfano, kirusi cha ebola cha nchini Uganda kinaitwa ‘Bundibugyo Virus’ na kile cha DRC kimepewa jina la ebola.
Kirusi cha nchini Sudan kimepewa jina la Sudan Virus na nchini Ivory Coast kimepewa jina la Tail Virus.
Aina ya tano ya kirusi cha ebola ilipatikana Amerika ya Kusini, lakini kirusi hiki hakijabainika kusababisha madhara kwa binadamu.

Ebola ilivyoingia duniani

Tukio la kwanza la ugonjwa hatari wa ebola liligundulika Agosti 29, 1976 katika eneo la nyanda za juu nchini DR Congo, liitwalo, Yambuku.
Ugonjwa huu uliwapata wakazi wa Yambuku ambao inasemekana walikuwa wakila mizoga ya wanyama wa porini, hasa sokwe na popo.
Mwaka huohuo ugonjwa huo uliibuka nchini Sudan katika maeneo ya viwanda vya pamba, katika Mji wa Nzara na mwaka 1994, ugonjwa huu uliibuka nchini Ivory Coast na kusababisha maafa makubwa.
Ugonjwa wa ebola uliibuka nchini Uganda Julai 2007 katika Wilaya ya Bundibugyo.

Binadamu hupataje ebola?

Utafiti uliofanyika miaka ya nyuma ulibaini kuwa virusi vya ebola huingia kwa mwanadamu kama tulivyosema hapo juu kutoka kwa wanyama wa porini, hasa sokwe na popo.
Baada ya binadamu kula nyama yenye virusi hivyo, husambaa katika mwili wake na huo ndiyo mwanzo wa wanadamu wengine kupata maradhi hayo.
Utafiti huo uligundua kuwa baadhi ya wanyama wanaweza kuishi na virusi vya Ebola bila kuwadhuru wanyama wengine japokuwa wengine huweza kudhurika na kufa kama wanavyoathiriwa wanadamu.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top