Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

SERENGETI BREWEIES, AIRTEL TANZANIA NA PUMA ZACHANGIA KUFANIKISHA WIKI YA NENDA KWA USALAMA BARABARANI

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Pereira Ame Silima (kushoto)akipokea sehemu ya ya stika maalum kwa ajili ya kampeni ya usalama barabarani toka kwa wadhamini wa stika hizo kwa mwaka huu Airtel na Puma, wanaokabidhi  (kutoka kulia) ni  Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel, Bi. Beatrice Singano na Mkurugenzi wa kampuni ya Mafuta Puma Bw. Maregesi Manyama. Anayeshuhudia  ni Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, SACP Mohamed Mpinga. Airtel Tanzania na Puma ni wadhamini wakuu wa wiki ya uhamasisaji wa wiki ya Nenda kwa usalama ambapo mwaka huu kitaifa itafanyika mkoani Iringa ikiwa imebeba ujumbe usemao “ Pambana na ajiali za barabarani kwa vitendo, zingatia sheria. 
Kamanda Mpinga akionyesha jinsi ya kufungua na kubandika stika hizo maaalum. Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, SACP Mohamed Mpinga akipokea msaada wa fulana 1000 za kuhamasisha wiki ya usalama barabarani na vipeperushi 500   kutoka kwa Mkurugenzi wa Mawasiliano wa kampuni ya bia ya Serengeti (SBL), Teddy Mpunda katika makabidhiano yaliyofanyika kwenye makao makuu ya Kikosi cha Usalama Barabarani jijini Dar es salaam. Kushoto ni Meneja wa Mipango Endelevu na Uwajibikaji kampuni ya Serengeti, Nandi Mwiyombela. Vifaa hivyo vina thamani ya shilingi milioni 17.5 na kampuni hiyo imesema inaangalia uwezekano wa kuchapisha vipeperushi vingine kwa ajili ya mkoa wa Dar es salaam ambapo hivi vya awali vitapelekwa mikoani.           
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright 2025 EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG | Designed By Code Nirvana
Back To Top