Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

WAKAZI WA MABWEPANDE WAZIDI KUNUFAIKA NA MISAADA MBALIMBALI

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam  Saidi Meck Sadiki(kulia) akipokea msaada wa vitu mbalimbali vilivyotolewa na watanzania waishio nchini Uingereza kuwasaidia wakazi wa Mabwepande walioathiriwa na mafuriko yaliyotokea mwezi Desemba 2011 jijini Dar es salaam leo. Wanaokabidhi msaada huo ni kutoka kushoto ni Awadh Salim mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Bw. Mohammed Abdulrahaman Meneja wa kampuni hiyo Tanzania na Bw. Chris  Lukosi, Mkurugenzi wa  Kampuni ya Usafrishaji wa Mizigo ya Serengeti.
Mkurugenzi wa  Kampuni ya Usafrishaji wa Mizigo ya Serengeti (Serengeti Freight Forwarders Ltd) Bw. Chris Lukosi akimkabidhi  Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam  Saidi Meck Sadiki(kulia) moja ya boksi lenye vitu mbalimbali vilivyotolewa na watanzania waishio nchini Uingereza kuwasaidia wakazi wa Mabwepande walioathiriwa na mafuriko yaliyotokea mwezi Desemba 2011 jijini Dar es salaam.
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam akiwaeleza jambo viongozi wa Kampuni ya Usafirishaji wa Mizigo ya Serengeti (Serengeti Freight Forwarders Ltd) iliyosafirisha bure msaada wa vitu mbalimbali vikiwemo viatu, nguo na vifaa vya watoto vilivyotolewa na watanzania waishio nchini Uingereza kuwasaidia wakazi wa mabwepande.
Viongozi wa kampuni ya ya Usafrishaji wa Mizigo ya Serengeti (Serengeti Freight Forwarders Ltd) Bw. Chris Lukosi wakiwa katika picha ya pamoja  na  Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam  Saidi Meck Sadiki (wa pili kutoka kulia) mara baada ya kukabidhi msaada wa vitu mbalimbali vilivyotolewa na watanzania waishio nchini Uingereza leo jijini Dar es salaam.
Picha na Aron msigwa – MAELEZO
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top