Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

WAKULIMA WALILIA MFUMO WA STAKABADHI GHARANI

PAMOJA na mfumo stakabadhi mazao ghalani kulalamikiwa na wakulima wa zao la korosho kuwa ndiyo chanzo kikubwa cha umasiki wao bado  Bodi  ya Korosho imedai kuwa mfumo huo ni mkombozi kwa wakulima.
 
Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Anna Margareth Abdallah, alisema hayo jijini Dar es Salaam jana, wakati wa uzinduzi wa msimu wa ununuzi wa korosho kwa mwaka 2012/13, unatarajiwa kuanza Septemba 20 mwaka huu, kama ilivyoamuliwa na mkutano mkuu wa Bodi hiyo uliyofanyika mkoani Morogoro hivi karibuni.
 
Alisema haamini kama kuna mkulima anayepinga mfumo huo, kama yupo basi atakuwa anamatatizo.
 
“Huu mfumo hauna matatizo bali matatizo yapo kwa baadhi ya watendaji ambao wanashindwa kuwajibika hivyo nawataka kumaliza kasoro hizo na kutoa elimu ya kutosha kwa wananchi kuhusu mfumo huu”alisema.
 
Akizungumzia kuhusu upangaji wa bei ya mkulima, Anna alisem upangaji huo umezingatia gharama halisi za uzalishaji pamoja na bei ya soko la korosho ghafi kimataifa.
 
Alisema baada ya kuzingatia maoni ya wadau, Bodi imeamuwa kuwa bei ya mkulima itakuwa Sh. 1,200 kwa kila kilo moja ya korosho ya daraja la kwanza (Standard Grade), Sh. 960 kilo moja ya daraja la pili (Under Grade), ambayo ni sawa na asilimia 80 ya bei ya daraja la kwanza.
 
Anna alibainisha kuwa mkulima atalipwa malipo ya kwanza asilimia 70 ya bei sawa na sh 850 baada ya kufikisha korosho katika maghala ya chama cha msingi, asilimia 30 sawa na sh 350 kwa kilo zitalipwa baada ya kuuzwa mnadani.
 
Aidha, mkulima atastahili malipo ya tatu ya majaaliwa endapo korosho yake itauzwa kwa bei nzuri.
 
Alitoa angalizo kuwa ni vyama vya ushirika tu kuwa ndivyo vitakavyoruhusiwa kukusanya korosho kutoka kwa wakulima.
 Anna alisisitiza kuwa korosho zote zitakazonunuliwa nje ya utaratibu huo zitakuwa zimepatikana kwa njia ya magendo (kangomba), na wahusika wote watachukuliwa hatua kali za kisheria.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright 2025 EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG | Designed By Code Nirvana