Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

UTARATIBU MPYA WA UBINGWA WA NGUMI ZA KULIPWA WA AFRIKA YA MASHARIKI NA KATI

Shirikisho la Ngumi za Kulipwa la Afrika ya Mashariki na Kati (ECAPBA) linapenda kuwatangazia mapromota, mameneja pamona na wadau wote wa ngumi katika ukanda huu kuwa kuanzia leo tarehe 4 Octoba 2012 ubingwa wote wa (ECAPBA) utaishi kwa kipindi cha miezi minne tu!
 Aidha, kuna taratibu mpya za kuandaa ubingwa wa ECAPBA na wale walio mabingwa mpaka sasa mwisho wa ubingwa wao ni mwezi wa 12. Baada ya hapo watatakiwa watetee ubingwa na taratibu mpya za ECAPBA.
 1.       Kuanzia sasa mabondia wote watakaogombea ubingwa wa ECAPBA ni lazima wawe wameshapigana mapambano yasiyopungua 8  mawili ya raundi 4, mawili ya raundi 6, mawili ya raundi 8 na mawili ya raundi 10.
2.       Kabla ya mpambano wenyewe ni lazima majina na rekodi za mabondia watakaocheza zikubaliwe na ECAPBA
3.       Waamuzi wote watakaosimamia mapambano haya ni lazima wapitishwe na ECAPBA
4.       ECAPBC haitaruhusu pambano kutangazwa kabla ya kupata kibali chake.
 Haya yote yanafanyika ili kulinda viwango na maisha ya mabondia pamoja na wadau wanaoshiriki katika kuuendeleza mchehzo wa ngumi z a kulipwa katika ukanda huu wa Afrika ya Mashariki na Kati.
Imetolewa na;
 Onesmo Alfred McBride Ngowi
Rais,
Shirikisho la Ngumi za Kulipwa la Afrika ya Mashariki na Kati (ECAPBA)
Dar-ES-Salaam, Tanzania
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top