Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

WAZIRI MULUGO: WANAFUNZI WANAFELI KWA UZEMBE WAO

 
NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo, amesema kufeli kwa baadhi ha wanafunzi kwenye mitihani ya taifa hakutokani na walimu kutokamilisha mitaala bali kunatokana na uzembe wa wanafunzi wenyewe.
 
Mulugo alitoa kauli hiyo wakati akitoa taarifa kwa Umma kuhusu mitihani ya kidato cha nne na mtihani wa maarifa inaotarajiwa kuanza Oktoba 8 hadi 25 mwaka huu.
 
Alisema wanafunzi wanaotoa madai hayo wengi wao ni wale waliyokuwa wakishindwa kuwasikiliza walimu wao wakati wakifundisha darasani.
 
“Kwa kawaida mfamaji haishi kutapatapa hivyo hao wanaosema hivyo mara nyingi ni wale waliyokuwa wakipata sifuri tangu awali”alisema Mulugo.
 
Akizungumzia mtihani huo wa kidato cha nne, Mulugo alisema jumla ya watahiniwa waliondikishwa kufanya mtihani huo ni 481, 414, wakiwemo vulana 263, 202 ambapo ni sawa na asilimia 54.67 huku wasichana wakiwa 218, 212 sawa na asilimia 45.33.
 
Alisema idadi hiyo ya watahiniwa wote walioandikishwa mwaka huu ni sawa na ongezeko la watahiniwa 31,090 hiyo ni sawa na asilimia 6.90 ikilinganishwa na watahiniwa 450,324 walioandikishwa mwaka jana.
 
Aliongeza kuwa watahiniwa wote waliondikishwa kufanya mitihani mwaka huu  wamegawanyika katika makundi matatu, ambayo ni watahiniwa wa Shule (School candidates), ni 412,594 wakiwemo wavulana  228,991 sawa na asilimia 55.50, wasichana 183,603 ambapo hiyo ni asilimia 44.50.
 
Mulugo alisema watahiniwa hao wa Shule mwaka huu ni ongezeko la watahiniwa 63,204 sawa na asilimia 18.09 ikilinganishwa na na watahiwa 349, 390 wa mwaka jana.
 
Alisema watahaniwa wakujitegeamea (Private candidates),  ni 68,820 wakiwemo wanaume 34,211 ikiwa hiyo ni sawa asilimia 49.71 na wanawake 34,609 ambapo hiyo ni asilimia 50.29.
 
Wengine ni  watahiniwa wakujitegemea walioandikishwa  mwaka huu ni pungufu ya watahiniwa 32,114 ikiwa ni upungufu wa asilimia 31.82 ikilinganishwa na watahiniwa 100, 934 walioandikishwa mwaka jana.
 
Akifafanua zaidi, alisema jumla wa mtihani wa maarifa walioandikishwa mwaka huu ni 21,314 wakiwemo wanaume 8,174 hiy0 ni asilimia 38.35 huku wanawake wakiwa 13,140 sawa na asilimia 61.65.
 
Mulugo alisema watahiniwa hao walioandikishwa mwaka huu ni pungufu  ya watahiniwa 8,133 sawa na asilimia 27.62 ikilinganishwa na watahiniwa 29,447 wa mwaka jana.
 
Wakati huo huo, alisema mwaka 2012/13 jumla ya wanafunzi 11,242 walichaguliwa kujiunga na mafunzo ya uwalimu,  ngazi ya cheti walikuwa 5,615 huku stashahada wakiw 5,627.
 Mulugo alisema hadi kufikia Agosti 30 mwaka huu jumla ya wanafunzi 4,395 ngazi ya cheti na 3,474 ngazi ya stashahada waloripoti vyuoni ambapo wanafunzi 1217 wa ngazi ya cheti na 2,153 stashahada hawakuripoti vyuoni halioifanya wizara kufanya uchaguzi wa pili.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top