Aliyekuwa
waziri wa Maliasili na utalii Bw Ezekiel Maige akitazama meno ya tembo
yaliyokamatwa na askari wa wanyamapori ,chini waliokamatwa ni majangili
Wizara ya Maliasili na utalii imeongeza idadi ya askari na silaha zitakazotumika kukabiliana na ujangili katika maeneo mbalimbali kwa lengo la kuhakikisha kuwa ujangili hauathiri maisha ya tembo na wanyama wengine nchini.
Wizara ya Maliasili na utalii imeongeza idadi ya askari na silaha zitakazotumika kukabiliana na ujangili katika maeneo mbalimbali kwa lengo la kuhakikisha kuwa ujangili hauathiri maisha ya tembo na wanyama wengine nchini.
Katika
kuhakikisha hilo Wizara imeweka utaratibu wa kupata matukio ya kila
siku kutoka vituo vyote vya hifadhi kuhusiana na ujangili wa wanyamapori
wote akiwemo tembo.
Wizara
pia inafuatilia taarifa za mienendo ya tembo chini ya Taasisi yake ya
Utafiti wa Wanyamapori (TAWIRI) kuanzia kipindi cha Mwaka 2010 hadi
2015. Kazi kubwa ya taasisi hii ni kupata taarifa
mbalimbali zinazohusiana na maisha ya tembo kwa kuangalia uzao,
mtawanyiko, maradhi, malisho na vifo vya tembo kwa ujangili, maradhi au
umri ikiwa ni pamoja na kufanya sense za wanyamapori wote.
Taarifa
za TAWIRI zinaonesha kuwa idadi ya tembo bado ni kubwa na vifo
vilivyoripotiwa vya ujangili bado viko kwenye kiwango cha kawaida.
George Matiko
MSEMAJI
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII


Post a Comment