Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MANTRA YAKABIDHI MRADI WA UMEME WA NISHATI YA JUA KWA SHULE YA SEKONDARI SELOUSS

 


Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Abdallah Lutavi akiwasha taa kuzindua mradi wa umeme wa nishati ya jua kwenye shule ya Sekondari Selous iliyopo Wilaya ya Namtumbo uliyofadhilwa na kampunin ya Mantra Tanzania kwa shilingi milioni 28.7. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mantra Tanzania Asa Mwaipopo na mbunge wa Namtumbo Vita Kawawa(wapili kushoto). (Na Mpiga Picha Wetu).
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mantra Tanzania Asa Mwaipopo (kulia) akifafanua jambo wakati wa hafla ya kukabidhi mradi wa umeme wa nishati ya jua kwenye shule ya Sekondari Selous iliyopo Wilaya ya Namtumbo. Wapili kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Abdallah Lutavi.
Mbunge wa Namtumbo Vita Kawawa(kushoto) akibadilisha mawazo na Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Abdallah Lutavi(katikati) wakati wa hafla ya kukabidhi mradi wa umeme wa nishati ya jua kwenye shule ya Sekondari Selous iliyopo Wilaya ya Namtumbo.Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mantra Tanzania Asa Mwaipopo.

Na Mwandishi Wetu, Namtumbo.

KAMPUNI ya Mantra Tanzania Limited imeikabidhi mradi wa umeme wa nishati ya jua wenye thamani ya shilingi milioni 28.7 kwa shule ya Sekondari ya Selous iliyopo Wilaya ya Namtumbo, Mkoani Ruvuma, utakaosaidia kuinua kiwango cha elimu katika shule hiyo.

Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi mradi huo jana, Mkurugenzi Mtendaji wa Mantra Tanzania Asa Mwaipopo alisema kuwa kampuni yake imejikita katika kusaidia miradi mbalimbali katika mkoa huo.

Mwaipopo alisema kuwa mradi utawasaidia wanafunzi wa shule hiyo kujisomea wakati wa usiku pamoja na kusaidia kufukuza wanyama wakali waliyopo eneo la shule hiyo.

“Baada ya kumalizika kwa mradi huu,tunaimani kuwa wanafunzi watapata fursa nzuri ya kujisomea katika mazingira tulivu. Tunamatarajio kuwa mradi huu utasaidia kuinua kiwango cha elimu cha shule hii na nimatarajio yetu kuwa utatunzwa vizuri kwa matumizi ya kizazi kijacho,” alisema Mwaipopo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo, Abdallah Lutavi aliyekuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa na mategemeo makubwa kuwa mradi huo na kusisitiza kuwa mradi huo utakuwa nguzo ya kuboresha elimu katika shule hiyo.

Lutavi alisema kuwa mradi huo utausaidia mpango madhubuti wa wilaya wa hiyo unaolenga kuhakikisha kuwa ifikapo Desemba 2013 kila shule katika wilaya hiyo inakuwa na maabara.

“Mpaka sasa, ni shule sita tu ndiyo zenye maabara. Lengo letu ni kuhakikisha kuwa shule zote katika wilaya zinakuwa na maabara. Maabara hizo haziwezi kukamilika bila umeme.

“Tunatoa shukrani zetu kwa Mantra Tanzania kwa mchango wao na tutahakikisha kuwa mradi unatunzwa vizuri,” alisema.

Aidha, Mbunge wa Namtumbo, Mh. Vita Kawawa wakati wa tukio hilo alitoa wito kwa uongozi wa wilaya kuhakikisha kuwa ujenzi wa mabweni ya wavulana unapewa kipaumbele wakati wa bajeti ya fedha ya wilaya ijayo.

“Wavulana wanalazimika kutembea mpaka kilometa tano hali ambayo inaweka maisha yao hatarini dhidi ya wanyama wakali. Ombi langu ni kuwa ujenzi wa mabweni ya wavulana upewe kipaumbele kikubwa katika bajeti inayofuata,” alisema.

Awali Mwalimu Mkuu Msaidizi wa shule, Bw. Henry Milanzi alibainisha kuwa shule yake inakumbwa na changamoto nyingi ikiwemo ukosefu wa maji safi na salama pamoja na kutokuwepo na ukuta katika eneo la shule.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright 2025 EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG | Designed By Code Nirvana