Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Mkutano Wa Mrejesho Halmashauri Ya Wilaya Wavunjika


 

Baadhi ya Madiwani wa halmashauri ya wilaya Singida wakiwa ukumbini
Kaimu mkuu wilaya Singid ambaye pia ni DC wa Ikungi, Manju Msambya akiahirisha mkutano wa marejesho uliofanyiwa tathimini
Wataalamu wa halamashauri wilaya SINGIDA wakisubiri kuanza mkutano wa marejesho ambao hata hivyo haukufanyika baada ya halmasha

MKUTANO wa mrejesho, juu ya ufuatiliaji na uwajibikaji kwa halmashauri wilaya Singida, juzi ulivunjika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo, baada ya taarifa kuonesha udhaifu mkubwa kwa miradi ya sekta ya afya.

Akiahirisha mkutano huo hadi desemba 17, 2012, kaimu mkuu wilaya Singida ambaye pia ni mkuu wa wilaya mpya ya Ikungi, Manju Msambya alisema utafiti uliofanywa na shirika la “SIKIKA”, la jijini Dar es Salaam, haujakamilika kutokana na halmashauri kutoipitia kwanza taarifa hiyo, ndipo iwasilishwe.

Hali ya hewa ilianza kuchafuka mapema saa nne asubuhi, baada ya watumishi wa shirika la SIKIKA kugawa taarifa kwa wajumbe wa mkutano huo, lakini ikionesha udhaifu mkubwa wa utekelezaji wa miradi ya halmashauri ya wilaya Singida, katika sekta ya afya.

Baada ya wajumbe (madiwani) na waalikwa, wakiwemo viongozi wa madhehebu ya dini kuipitia taarifa hiyo kabla ya kikao kufunguliwa rasmi, ndipo manung’uniko yalianza, huku baadhi ya madiwani wakidai miradi mingi kwenye maeneo yao imechakachuliwa.

Hali hiyo ililazimu wataalamu kutoka ukumbini kwenda kufanya kikao cha dharula kilichogharimu zaidi ya saa tatu, chini ya mkuu wa wilaya Ikungi, Manju Msambya na mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, Illuminata Mwenda, na kuchukua uamuzi wa kuahirisha mkutano huo, hadi Desemba 17, mwaka huu.
Akitangaza uamuzi wa kuahirisha, Msambya alisema baada ya kupitia taarifa hiyo, wamebaini kuna baadhi ya vitu muhimu havikuorodheshwa, hivyo halmashauri nayo inapaswa kuipitia kabla ya kuwasilishwa kwa wajumbe.

“Wenzetu wa Sikika tumechukua muda mrefu sana kuwashawishi kuahirisha, kwa sababu wana maeneo mengi ya kufanya shughuli hizi..sasa nikuombeni radhi na kuahirisha hiki kikao, muungwana anapoomba kwa muungwana mwenzake, husikilizwa…kuna mambo yamepungua,”alisema Msambya.
Msambya alisema kuna baadhi ya vipengele havijafanyiwa kazi vizuri, na kukosea ni jambo la kawaida kwa kila binadamu.

Hata hivyo kauli hiyo iliamsha hisia kali kwa baadhi ya madiwani, akiwemo Teddy Augustino Daghau, kata Ikungi (CHADEMA),aliyedai mkutano huo umelazimika kuahirishwa kutokana na taarifa ya SIKIKA kukosoa utekelezaji wa miradi mingi sekta ya afya, wilaya ya Singida.

Teddy alisikitishwa na hali hiyo iliyojitokeza, na kushutumu wazi ofisi ya mkuu wa wilaya na mkurugezi mtendaji wa halmashauri ya wilaya hiyo, hali inayotoa viaashiria vya ufujaji mkubwa wa fedha za umma sekta ya afya, na ameiomba serikali kuingilia kati na kufuatilia kwa kina sakata hilo.

Akiongea na waandishi wa habari nje ya ukumbi baada ya mkutano huo kuahirishwa, mratibu wa shughuli za SIKIKA, Mahindi Zakayo kutoka Dar es Salaam alisema kazi ya ufuatiliaji sekta ya afya wilayani Singida, ilianza wiki nne zilizopita na kushirikisha wadau wote wa afya, wakiwemo pia madiwani.

Alisema madiwani hao walielekezwa mifumo mbalimbali jinsi inavyofanya kazi katika halmashauri yao, kwa lengo la kufanikisha uwajibikaji, usimamizi wa raslimali za halmashauri, utendaji na ufuatiliaji.

“Kimsingi timu imefanya kazi zake, imeangalia mipango ya halmashauri, mgawanyo wa raslimali, matumizi na utendaji….lakini pia timu zinazofuatilia utendaji kuona je zote zinafanya kazi ya kuhudumia jamii?, sasa kwa bahati mbaya mrejesho siku hii ya leo haukuweza kufanyika,”alieleza kwa masikitiko Mahindi.
Alisema binafsi hakuona tatizo lolote kubwa, kwani kimsingi wajumbe wailikuwa wapokee taarifa ya kazi nzima iliyofanyika katika hatua tano ila halmashauri wamedai hawajazipitia hoja, badala ya kupokea na kuzinfanyia kazi baadaye, hapo ndipo tofauti iliyotokea.

Mahindi alisema haoni tatizo lolote lililojitokeza hadi mrejesho huo usifanyike, badala ya kukubali kwanza hoja na baadaye ndipo zifanyiwe kazi
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top