Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

My Everything ya Alikiba yasikika redioni


 

Na Elizabeth John
BAADA ya kukaa kimya kwa muda mrefu, Mkali wa muziki wa kizazi kipya nchini Ali Kiba baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu ameachia kibao chake kipya kinachokwenda kwa jina la ‘My everything’.

Akizungumza na Habari Mseto jijini Dar es Salaam, Alikiba amesema alikuwa kimya kwa muda mrefu sasa amejipanga na ameamua hivyo mashabiki wakae tayari kupokea burudani kutoka kwake.

“Nilikuwa kimya kwa muda mrefu sasa nimejipanga na nimeamua kutoa burudani kwa mashabiki wangu hivyo watarajie vitu vizuri mfurulizo kutoka kwangu,” amesema Alikiba.

Amesema sasa anatarajia kutoa vitu mfululizo kwaajili ya kuwapa burudani mashabiki wake na kudai kuwa baada ya wiki mbili mbele atakuwa ameanza kusambaza video ya kibao hicho.

“Kkwasasa ukichelewesha kutoa video wimbo unachuja haraka hivyo [sipo tayari kuaribu kazi yangu nimejipanga na nimeamua ntaakikisha video inatoka mapema kabla ya kibao hicho kuchuja,” amesema Alikiba.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top