Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

SHARO MILIONEA KUZIKWA LEO TANGA, WADAU WAMLILIA

 


MSANII Hussein Ramadhani Mkiete anatarajiwa kuzikwa leo nyumbani kwao, Tanga.
Kwa mujibu wa Diwani Makame Seif ambaye ni rafiki wa karibu marehemu, aliyefarfiki kwa ajali Saa 2:00 usiku jana eneo la Maguzoni Tanga, Polisi wametambua ni Sharo Millionea kwa vitambulisho vyake na picha moja ya passport aliokuwa nayo mfukoni ambavyo kwa sasa viko na polisi.
Diwani huyu amemfahamisha mwandishi kuwa Sharo Millionea ameumia vibaya sana kichwani, kifuani na kwenye mikono. Pia Mjomba wa marehemu amethibitisha kuwa Sharo Millionea atazikwa Tanga na asubuhi ya leo ratiba ya msiba itatolewa. Ndugu na marafiki wa Sharo wameanza kwenda hospitalini baada tu ya taarifa hizi kuwafikia. Familia ya Sharo imeshafika Hospitali ya Teule ya Tanga.


Wadau mbali mbali wa tasinia ya burudani wameonyesha kusikitika na kuhuzunishwa na kifo cha msanii mahiri wa vichekesho nchini Sharomilionea
KITALE akihojiwa na TBC akiongea akiwa na majonzi ya hali juu alisemaa alishindwa kuamini kama kweli sharo kafariki mpaka alipompigia simu mzee majuto nakumthibitishia kweli tukio ndo hilo aliishiwa nguvu baada ya kuthibitishiwa habari nakusema amempoteza mtu mhimu sana kwake binafsi na hajui itakuwaje.na alishindwa kujizuia kulia

Steve nyerere nae alipohojiwa na TBC nae alionyesha kusikitishwa na kifo cha msanii huyo nakusema ameacha pengo kubwa katika tasnia hiyo ya comedy

 Jackson Mbando wa airtel akiongea na clouds fm katika kipindi cha power breakfast alisema kuwa nipigo kubwa katika tasnia zima ya burudani na airtel wameskitishwa na kuumia sana kutokana na kifo cha msanii huyo ukizingatia alikuwa mdau wao mkubwa amnetegeneza matamngazo na airtel

 


R.I.P SHARO MILLIONEA
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top