Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

SHIRIKA LA CEF LAANZISHA MPANGO WA KUPUNGUZA TATIZO LA AJIRA

 

SHIRIKA lisilo la kiserikali linaloshughulika na kuinua hali ya maisha ya masuala ya kielimu,kiuchumi na kiafya la ‘Community Educational Foundation’ (CEF) limeanzisha mpango wa kupunguza tatizo la ajira kwa vijana unaojulikana kama ‘kazi nje nje’

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa CEF John Shusho, alisema programu ya kazi nje nje yenye lengo la kuelimisha vijana juu ya stadi za ujasiriamali, imeasisiwa na Shirika la Kazi Duniani(ILO) na hapa nchini inafanya kazi kwa ushirikiano wa karibu na Wizara ya Kazi na Maendeleo ya Vijana pamoja na Wizara ya Utumishi.

Alisema mpango huo wa Kimataifa utatekelezwa hadi Mwaka 2014 katika mikoa ya Tanga, Tabora, Singida, Mwanza, Mbeya, Pwani, Lindi na Mtwara, ambapo pia unaendeshwa katika nchi za Kenya na Uganda.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo, stadi hizo ni kuwajengea uwezo wa kijasiriamali, kubuni wazo la Biashara, kuandaa andiko na kuanzisha biashara zitakazowawezesha kukabiliana na hali ngumu ya maisha.

Shusho alisema makundi lengwa katika program hiyo ni pamoja na vijana wasio na ajira, wafanyabiashara katika sekta zisizo rasmi na vikundi vya uzalishaji mali vilivyopo katika maeneo ya mikoa hiyo.

Alitanabaisha kuwa moja ya mambo yanayopewa kipaumbele na CEF ni kutoa changamoto kwa walengwa kutobweteka na kuwaachia wageni kuendelea kutumia fursa nyingi za kazi zilizojaa kwenye maeneo yao husika na nchini kwa ujumla.

“Tayari ILO imeshatoa mafunzo kwa wakufunzi kutoka CEF ambao jukumu lao litakuwa ni kuibua na kuchechemua vipaji vya kazi miongoni mwa vijana ambao wengi wao wamekaa vijiweni bila kujua la kufanya” alisema Shusho.


Kwa mujibu wa Shusho, rekodi za Shirika la Taifa la Twakwimu (NBS), zinaonesha takwimu za mwaka 2006, kiwango cha ukosefu wa ajira miongoni mwa vijana kilikuwa ni wastani wa asilimia 13.4 kwa vijana, idadi aliyosema ni kubwa ukilinganisha na idadi ya vijana iliyokuwepo wakati huo.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top