Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

UVCCM YAGOMA KUTUMIWA KAMA NGAZI NA WAKIMBILIA IKULU

UMOJA wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), umekunjua makucha na kuwapiga marufuku vigogo wanaowania urais kupitia chama hicho, kuwatumia kama ngazi ya kufanikisha malengo yao.
Akihutubia mkutano wa hadhara kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Kaluta jana, Mwenyekiti wa UVCCM, Sadifa Hamis Juma alisema kuna baadhi ya vigogo wenye malengo ya kuwania nafasi ya urais wanawagawa vijana.
Mkutano huo ulihudhuriwa na vigogo wa chama hicho akiwamo Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa na baadhi ya mawaziri.
UVCCM wamekuwa wakituhumiwa kutumiwa na vigogo walio katika mbio za kuwania urais mwaka 2015.
Wakati wa uchaguzi wa ndani wa chama hicho, imekuwa ikielezwa kuna wagombea urais waliokuwa wakihaha kuhakikisha nafasi za uongozi wa jumuiya hiyo zinachukuliwa na vijana wanaowaunga mkono. Sadifa alisema makundi yaliyokuwapo kabla na baada ya uchaguzi wa jumuiya hiyo, sasa yanatakiwa kuvunjwa na kujenga umoja huo kwa masilahi ya chama.
Alisema kitendo cha wanaotaka urais kuwatumia vijana kama ngazi, sasa watambue kuwa hawapo tayari kwa hilo.

Chanzo: Mwananchi
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top