Wadau na
Makampuni mbali mbali Zanzibar wameombwa kuichangia Taasisi ya ‘Cooperation for
assisting handicapped people’ inayojishughulisha na kusaidia watu
wasiojiweza ili Taasisi hiyo iweze kujenga Mabweni ya Shule mbili za kata Temeke
Jijini Dar es Salaam.
Ombi
hilo limetolewa na Mkurugenzi mtendaji wa Kampuni hiyo Mhina Michael Shengena
wakati alipokuwa akizungumza na Waandishi wa Habari katika Ukumbi wa Idara ya
Habari Maelezo Rahaleo Mjini Zanzibar.
Amesema
wanahitaji wasaidiwe Sh Milioni Arobaini (40,000,000) ndani na nje ya Zanzibar
kwa ajili ya ujenzi wa Mabweni ya watoto Yatima,Walemavu na Watoto wanaoishi
katika mazingira hatarishi ili waweze kupata taaluma ambayo itawasaidia katika
maisha yao.
Amezitaja
Shule ambazo wana mpango wa kujenga mabweni kwa wanafunzi hao kuwa ni Nguva na
Sumangira zilizopo katika Manispaa ya Temeke Jijini Dar es
Salaam.
Aidha
ametaja njia ambayo Wadau mbalimbali wanaweza kuchangia msaada wao kwa Kampuni
hiyo kufanikisha ujenzi huo kuwa ni kupitia akauti namba 01J2070153800 ya CRDB
Bank.
Mkurugenzi
Mhina ameongeza kuwa watakuwa na ziara ya nchi nzima ambapo wanatarajia kukutana
na Viongozi wa Serikali, Siasa, Dini na Wananchi mbali mbali katika kuitangaza
Taasisi yao ili wadau waweze kuifahamu na
kuichangia.
Aidha
ametoa wito wa wananchi wa Zanzibar kushiriki katika harambee ya kuichangia
Taasisi yao itakayofanyika Ukumbi wa Hoteli ya Bwawani January 30, mwaka 2013
mjini Zanzibar.
Taasisi
ya ‘Cooperation for assisting handicapped people’ yenye Makao Makuu yake Mkoani
Iringa imesajiliwa mwaka 1998 chini ya Sheria za makampuni ya Tanzania Bara na
kupewa namba za usajili 3388 ambapo shughuli yake kuu ni kusaidia watu
wasiojiweza.
Wadau na
Makampuni mbali mbali Zanzibar wameombwa kuichangia Taasisi ya ‘Cooperation for
assisting handicapped people’ inayojishughulisha na kusaidia watu
wasiojiweza ili Taasisi hiyo iweze kujenga Mabweni ya Shule mbili za kata Temeke
Jijini Dar es Salaam.
Ombi
hilo limetolewa na Mkurugenzi mtendaji wa Kampuni hiyo Mhina Michael Shengena
wakati alipokuwa akizungumza na Waandishi wa Habari katika Ukumbi wa Idara ya
Habari Maelezo Rahaleo Mjini Zanzibar.
Amesema
wanahitaji wasaidiwe Sh Milioni Arobaini (40,000,000) ndani na nje ya Zanzibar
kwa ajili ya ujenzi wa Mabweni ya watoto Yatima,Walemavu na Watoto wanaoishi
katika mazingira hatarishi ili waweze kupata taaluma ambayo itawasaidia katika
maisha yao.
Amezitaja
Shule ambazo wana mpango wa kujenga mabweni kwa wanafunzi hao kuwa ni Nguva na
Sumangira zilizopo katika Manispaa ya Temeke Jijini Dar es
Salaam.
Aidha
ametaja njia ambayo Wadau mbalimbali wanaweza kuchangia msaada wao kwa Kampuni
hiyo kufanikisha ujenzi huo kuwa ni kupitia akauti namba 01J2070153800 ya CRDB
Bank.
Mkurugenzi
Mhina ameongeza kuwa watakuwa na ziara ya nchi nzima ambapo wanatarajia kukutana
na Viongozi wa Serikali, Siasa, Dini na Wananchi mbali mbali katika kuitangaza
Taasisi yao ili wadau waweze kuifahamu na
kuichangia.
Aidha
ametoa wito wa wananchi wa Zanzibar kushiriki katika harambee ya kuichangia
Taasisi yao itakayofanyika Ukumbi wa Hoteli ya Bwawani January 30, mwaka 2013
mjini Zanzibar.
Taasisi
ya ‘Cooperation for assisting handicapped people’ yenye Makao Makuu yake Mkoani
Iringa imesajiliwa mwaka 1998 chini ya Sheria za makampuni ya Tanzania Bara na
kupewa namba za usajili 3388 ambapo shughuli yake kuu ni kusaidia watu
wasiojiweza.


Post a Comment