RAIS Jakaya Kikwete
amewataka Watanzania kujivunia na kuyaenzi mafanikio ya kisiasa, kiuchumi na
kijamii, yaliyopatikana tangu nchi ilipojipatia uhuru wake mwaka
1961.
Akizungumza kwenye
maadhimisho hayo ya mika 51 ya uhuru wa Tanzania Bara, uliofanyika kwenye uwanja
wa Uhuru jijini Dar es Salam leo, Rais Kikwete alisema yamekuwa tofauti na ya
awali, safari hii yakihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kuu kutoka nchi 14 za
Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC).
Alisema mafanikio hayo
yametokana na uvumilivu wa kisiasa ujengeka miongoni mwa
Watanzania.
Kikwete alisema katika
miaka 51 ya uhuru wa nchi hiyo, imekuwa katika utulivu na amani ambapo utulivu
huo umekuwa chachu ya maendeleo katika jamii ya
Watanzania.
Aidha, viongozi
waliohudhuria maadhimisho hayo, Rais Kikwete amewataja kuwa ni pamoja Rais wa
Jamhuri ya Congo (DRC), Joseph Kabange Kabila, Emilio Armando Guebuza,
(Msumbiji), na Hifikepunye Pohamba (Namibia), mbaye alishuhudia Tanzania Bara
ikipata uhuru mwaka 1961 na Makamu wa Rais wa Zambia Guy
Scott.
Wengine ni Makamu wa Rais
wa Angola Manuel Domingos, Waziri Mkuu wa Rwanda, Pierre Au Moyen, Waziri Mukuu
wa Swazland, Sibusiso Dlamini, Simba rashe na wengine.
Katika sherehe za
maadhimisho hayo kulikuwa na burudani mbalimbali ikiwemo gweride la vikosi vya
Majeshi, Halaiki ya watoto na ngoma za asili pamoja na kikundi cha Taifa cha
ngoma za asili kutoka Rwanda.
Naye Katibu wa Itikadi na
Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye amekiri kuwa miaka 51 ya uhuru
bado nchi inakabiliwa na changemoto mbalimbali ingawa yapo mafanikio katika
huduma nyingi za kijamii.
Pia amevitaka vyama
mbalimbali vya siasa kutobeza kila mafanikio yaliyopatikana katika nchi hiyo
bali vijaribu kuja na njia mbadala zitakazolisaidia taifa katika kuwakwamua
wananchi katika changamoto hizo kwani maendeleo ni ya Wanzania wote
.
Alisema serikali hii
imefanya mambo makubwa katika upande wa elimu pamoja na miundombinu ya barabara
hivyo ni vyema ikapongezwa.
Kwa Upande wake Mwenyekiti
wa Chama cha Mageuzi (NCCR Mageuzi), James Mbatia pamoja na kusherehekea miaka
51 bado inchi inakabiliwa na changamoto ya umasikini uliyopitiliza na kuwa
ufukara.
Alisema asilimia 30 ya
watanzania bado wanakula mlo mmoja kutokana na kukabiliwa na ufukara hivyo kuna
ulazima kwa serikali kuwekeza zaidi kwenye elimu kama chachu ya kuwakwamua
wananchi hao katika kuondokana na ufukara huo.
Katika hatua nyingine ya
maadhimisho hayo ya miaka 51 ya uhuru, Rais Kikwete ametoa msamaha kwa wafungwa
3814.
Akizungungumza kwa niaba ya
Rais, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi, alisema Rais
ametumia madaraka aliyopewa chini ya Ibara ya 45(1), ya Katiba ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania.
Aliwataja wafungwa
walionufaika na msamaha huo kuwa ni pamoja na wale wanotumikia kifungo
kisichozidi miaka mitano ambao hadi Desemba 9 mwaka huu wamekwishatumikia robo
ya vifungo vyao.
Wengine ni wagonjwa wa
Ukimwi, kifua kikuu, (TB),saratan na kundi la wafungwa wa wanawake walioingia
gerezani wakiwa na ujauzito na wale walioingia wakiwa na watoto wanaonyonya na
wasiyonyonya.
Dk Nchimbi aliongeza kuwa
kundi jingine ni la wafungwa wenye ulemavu wa mwili na
akili.
Aidha msamaha huo wa Raisi
hautawahusu wafungwa waliohukumiwa kunyingwa, wanaotumikia kifungo cha maisha,
wa makosa ya kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya kama vile cocaine,
heroine, bangi na mengine.
Wengine ni wafungwa
wanaotumikia kifungo kutokana na makosa ya kupokea au kutoa rushwa na wa makosa
ya kunajisi, ubakaji, kulawiti, makosa ya unyang’nyi wa kutumia silaha na wale
waliopatikana na hatia ya kuwapa mimba wanafunzi wa shule za mzingi na sekondari
ambao walitenda kosa hilo wakiwa na umri wa miaka 18.
Post a Comment