Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

DK JAKAYA KIKWETE AWATAKA WATANZANIA KUJIVUNIA MAFANIKIO YA UHURU KISIASA NA KIUCHUMI

RAIS Jakaya Kikwete amewataka Watanzania kujivunia na kuyaenzi mafanikio ya kisiasa, kiuchumi na kijamii, yaliyopatikana tangu nchi ilipojipatia uhuru wake mwaka 1961.
Akizungumza kwenye maadhimisho hayo ya mika 51 ya uhuru wa Tanzania Bara, uliofanyika kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salam leo, Rais Kikwete alisema yamekuwa tofauti na ya awali, safari hii yakihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kuu kutoka nchi 14 za Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC).
Alisema mafanikio hayo yametokana na uvumilivu wa kisiasa ujengeka miongoni mwa Watanzania.

Kikwete alisema katika miaka 51 ya uhuru wa nchi hiyo, imekuwa katika utulivu na amani ambapo utulivu huo umekuwa chachu ya maendeleo katika jamii ya Watanzania.
Aidha, viongozi waliohudhuria maadhimisho hayo, Rais Kikwete amewataja kuwa ni pamoja Rais wa Jamhuri ya Congo (DRC), Joseph Kabange Kabila, Emilio Armando Guebuza, (Msumbiji), na Hifikepunye Pohamba (Namibia), mbaye alishuhudia Tanzania Bara ikipata uhuru mwaka 1961 na Makamu wa Rais wa Zambia Guy Scott.
Wengine ni Makamu wa Rais wa Angola Manuel Domingos, Waziri Mkuu wa Rwanda, Pierre Au Moyen, Waziri Mukuu wa Swazland, Sibusiso Dlamini, Simba rashe na wengine.
Katika sherehe za maadhimisho hayo kulikuwa na burudani mbalimbali ikiwemo gweride la vikosi vya Majeshi, Halaiki ya watoto na ngoma za asili pamoja na kikundi cha Taifa cha ngoma za asili kutoka Rwanda.
Naye Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye amekiri kuwa miaka 51 ya uhuru bado nchi inakabiliwa na changemoto mbalimbali ingawa yapo mafanikio katika huduma nyingi za kijamii.

Pia amevitaka vyama mbalimbali vya siasa kutobeza kila mafanikio yaliyopatikana katika nchi hiyo bali vijaribu kuja na njia mbadala zitakazolisaidia taifa katika kuwakwamua wananchi katika changamoto hizo kwani maendeleo ni ya Wanzania wote .
Alisema serikali hii imefanya mambo makubwa katika upande wa elimu pamoja na miundombinu ya barabara hivyo ni vyema ikapongezwa.
Kwa Upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Mageuzi (NCCR Mageuzi), James Mbatia pamoja na kusherehekea miaka 51 bado inchi inakabiliwa na changamoto ya umasikini uliyopitiliza na kuwa ufukara.
Alisema asilimia 30 ya watanzania bado wanakula mlo mmoja kutokana na kukabiliwa na ufukara hivyo kuna ulazima kwa serikali kuwekeza zaidi kwenye elimu kama chachu ya kuwakwamua wananchi hao katika kuondokana na ufukara huo.
Katika hatua nyingine ya maadhimisho hayo ya miaka 51 ya uhuru, Rais Kikwete ametoa msamaha kwa wafungwa 3814.
Akizungungumza kwa niaba ya Rais, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi, alisema Rais ametumia madaraka aliyopewa chini ya Ibara ya 45(1), ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Aliwataja wafungwa walionufaika na msamaha huo kuwa ni pamoja na wale wanotumikia kifungo kisichozidi miaka mitano ambao hadi Desemba 9 mwaka huu wamekwishatumikia robo ya vifungo vyao.
Wengine ni wagonjwa wa Ukimwi, kifua kikuu, (TB),saratan na kundi la wafungwa wa wanawake walioingia gerezani wakiwa na ujauzito na wale walioingia wakiwa na watoto wanaonyonya na wasiyonyonya.
Dk Nchimbi aliongeza kuwa kundi jingine ni la wafungwa wenye ulemavu wa mwili na akili.
Aidha msamaha huo wa Raisi hautawahusu wafungwa waliohukumiwa kunyingwa, wanaotumikia kifungo cha maisha, wa makosa ya kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya kama vile cocaine, heroine, bangi na mengine.
Wengine ni wafungwa wanaotumikia kifungo kutokana na makosa ya kupokea au kutoa rushwa na wa makosa ya kunajisi, ubakaji, kulawiti, makosa ya unyang’nyi wa kutumia silaha na wale waliopatikana na hatia ya kuwapa mimba wanafunzi wa shule za mzingi na sekondari ambao walitenda kosa hilo wakiwa na umri wa miaka 18.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top