Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Dkt. Ali Mohamed Shein, Afanya Uteuzi Wa Wenyeviti Wa Bodi Mbali Mbali


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein ,amefanya uteuzi wa Wenyeviti wa Bodi mbali mbali katika Wizara ya Ardhi,Makaazi,Maji na Nishati,Zanzibar.
Dkt Shein amemteuwa Ashrak Mahmoud Hamid kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili,Wasanifu,Wahandisi na Wakadiriaji Ujenzi,Zanzibar. Kwa mujibu wa taarifa iliotolewa na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi,Dkt Abdulhamid Yahya Mzee amesema kuwa uteuzi huo wa Rais ameufanya kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya kifungu cha 4(1)(a) cha Sheria ya Bodi ya Wakandarasi Namba 5 ya mwaka 2008.
Aidha Dkt Shein amemteuwa Rama Keis Mgeni kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakandarasi, Zanzibar.Rais amefanya uteuzi huo kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya kifungu cha 5(1)(a) cha Sheria ya Bodi ya Wakandarasi Namba 6 ya mwaka 2008.
Uteuzi huo umeanza jana tarehe 12/12/2012.
IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top