Owino
Uhuru
Suleiman
Hatimaye beki mahiri wa azam fc
george owino amerejea ktk klabu yake ya zaman,simba
sc.
Aidha kiungo mahiri
wa simba,uhuru suleiman naye ametua azam fc baada ya timu hizo kubadilishana
wachezaji.
Habari za uhakika kutoka Azam
zinaeleza kwamba zoezi hilo limekamilika baada ya kukamilisha mchakato na tayari
uhuru ameshaanza mazoezi na wenzake.
Kiongozi huyo
aliongeza kuwa owino ambaye kwa sasa yupo mapumzikoni kwao kenya ätajiunga na
wekundu hao pindi atakaporejea nchini.
Ikumbukwe kuwa owino alipata
Kuichezea simba miaka miaka miwili iliyopita kabla ya kuumia goti na kwenda
kujitibia kwao ndipo azam ilipomsajili na kumpeleka india kwa matibabu
zaidi.
Katika hatua nyingine simba ipo
katika mazungumzo na azam fc ili kuweza kumchukua kwa mkopo nyota wake,agrey
morris ambaye kwa sasa anatumikia adhabu ya kusimamishwa kwa muda usiojulikana
kwa madai ya kuihujumu timu hiyo.
Simba ambayo ilimaliza mzunguko
wa kwanza wa ligi kuu bara ikiwa nafasi ya tatu kwsa sasa ipo katika kuimarisha
kikosi chake
Post a Comment