Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete leo mchana
ametunuku nishani kwa watu kutoka makundi mbalimbali yajamii waliotumikia taifa
kwa uadilifu na kutoa mchango wa pekee.Miongoni wa waliotunukiwa nishani leo ni
pamoja na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue ,Jaji Mstaafu wa Mahakama ya
Rufaa Eusebia Munuo pamoja na Msanii Mkongwe Bi.Fatma Baraka Khamis(Bi.Kidude)
Pichani juu.Wengine waliotunikiwa nishani ni pamoja na Watumishi wa umma na
askari jeshi na polisi
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza
la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Bi Fatma
Baraka Khamis,(Kidude) baada ya kutunukiwa nishani ya Sanaa na
Michezo na Rais wa Tanzania Dk.Jakaya Mrisho Kikwete,(kulia)
katika sherehe za kutunuku Nishani katika Viwanja vya Ikulu Dar
es Salaam.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza
la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Bi Fatma
Baraka Khamis,(Kidude) baada ya kutunukiwa nishani ya Sanaa na
Michezo na Rais wa Tanzania Dk.Jakaya Mrisho Kikwete,(kulia)
katika sherehe za kutunuku Nishani katika Viwanja vya Ikulu Dar
es Salaam,(katikati)Rais Mstaafu wa Tanzania Mzee
Mwinyi.
Rais Jakaya Kikwete akimpongeza Jaji Mstaafu Eusebia Munuo akivishwa nishani baada ya kumvisha nishani yake leo |
|
Post a Comment