Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MAISHA PLUS YAMKUTANISHA IBRAHIM NA NDUGU ZAKE, ALITELEKEZWA NA MAMA YAKE AKIWA MCHANGA

Ibrahim Matebu akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es salaam mara baada ya kukutanishwa na ndugu zake kufuatia kipindi cha Maisha Plus kumhoji na kuelezea matatizo yake mara baada ya kutelekezwa na mama yake Hedinesta Kileo kwenye basi mpakani mwa Tanzania na Kenya, ambapo kijana huyo akiwa bado mchanga aliokotwa na mama wa Kisomali ambaye alimlea mpaka alipofikisha miaka minne na yeye akamtelekeza , ndipo alipochukuliwa na serikali ya kenya akalelewa na kusoma huko.

Ibrahim alirudi nchini kwa kumfuata rafiki yake hakumtaja jina ambaye inadaiwa ni mkenya wakawa wanaishi mkoani Arusha, na ndipo alipofanikiwa kuingia katika kuwania nafasi ya kushiriki katika Shindano la Maisha Plus, hata hivyo hakufanikiwa kupita katika mchujo huo.
Mama mkubwa wa Ibrahim alimfananisha Ibrahim na mshindi wa pili wa Maisha Plus Venance Mushi ambaye ukiangalia kwa kiasi wanafanana, kutokana na historia aliyoitoa Ibrahim jambo lililompa mashaka kwani mdogo wake Hedinesta aliwahi kuwa na mimba lakini haikujulikana kilitokea nini mara baada ya kukimbia nyumbani kwao Arusha na kwenda kwa dada yake huko mpakani mwa kenya na Tanzania ambako inadaiwa alijifungua na baada ya mwezi mmoja akumtelekeza mtoto huyo, aliyeshika kipaza sauti ni Emanuel Anderson ndugu yake na Ibrahim
Kutoka kulia ni Emmanuel Anderson ndugu yake na Ibrahim, Ibrahim Mwenyewe na Venance Mushi ambaye ni mshindi wa pili wa Maisha Plus.
Mama Mkubwa wa Ibrahim akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dares salaam mara baada ya kukutana na mwanaye huyo ambaye ni mtoto wa mdogo wake Hedinesta Kileo, ambapo ameishukuru Maisha Plus kwa kumkutanisha na mtoto wake, lakini pia akaomba radhi kwa wazazi wa Venace Mushi na Venance mwenyewe kwa usumbufu uliotokea baada tukio hilo la kumfananisha mtoto wao Ibrahim na Venance kutokana na matukio yaliyomkuta Ibrahim akiwa bado mdogo
Mkurugenzi wa Maisha Plus Masoud Kipanya akizungumzia sakata hilo ambapo amesema Maisha Plus mbali ya kazi yake ya kawaida kama shindano, lakini imemkutanisha Ibrahim na ndugu zake na akasema kumbukumbu za picha zimetusaidia kujua ukweli wa jambo lenyewe kuhusu sakata la Ibrahim.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top