Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Ndege za Japan zajibu "tisho" la Uchina

 

Ndege ya kivita ya F-15
Ndege ya kivita ya F-15
Japan imeziamuru ndege zake za kivita zipae angani baada ya ndege ya serikali ya Uchina kuingia katika anga ya visiwa vya Bahari ya Mashariki mwa Uchina kwa muda, duru rasmi zimesema.
Msemaji wa serikali Osamu Fujimura alisema kuwa Japan iliamuru ndege za kivita za aina ya F-15 zipae angani wakati ndege hiyo ya Uchina ilipoonekana.

Tukio hilo lilipotokea tu, Japan "iliilalamikia" Uchina “mara moja”, shirika la habari la Kyodo lilimnukuu akisema.
Visiwa hivyo, vinavyojulikana kama Senkaku nchini Japan na Diaoyu nchini Uchina, vimegombaniwa na nchi hizo mbili kwa muda mrefu sasa.
Safari ya kawaida
Walinzi wa baharini wa Japan nao pia walisema kwamba meli za Uchina zinazofanya uchunguzi nazo zilionekana karibu na visiwa hivyo mapema siku hiyo.
Kwa upande wake, Uchina imesema kwamba safari ya ndege yake hiyo ni jambo la kawaida.
Japan ndiyo inayomiliki visiwa hivyo, ambavyo pia Taiwan inadai ni vyake.
Apple iPhone 5 yaonyesha ramani ya visiwa tataBahari inayozunguka visiwa hivyo ina samaki wengi na pia inadhaniwa kwamba ina mafuta.
Mmiliki
Japan ilitwaa visiwa vitatu kutoka kwa mmiliki Mjapani wa kibinafsi mnamo mwezi Septemba, lakini kitendo hicho kilizua malalamishi ya kidiplomasia na kutoka kwa raia nchini Uchina.
Tangu hapo, meli za Kichina zimekuwa zikionekana katika eneo la visiwa hivyo, jambo ambalo limeisababisha Japan kutoa onyo mara kwa mara

Chanzo: BBC Swahili
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top