Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

NIT KUANZAISHA MITAALA MIPYA YA WATAALAMU WA UCHUKUZI

CHUO cha Usafirishaji (NIT), kwa mara ya kwanza kinaanzisha mitaala mipya ya mafunzo ya wataalamu wa uchukuzi na usafirishaji mbayo italisaidia taifa kuondokana na uhaba wa wataalamu katika sekta ya uchukuzi na usafirishaji nchini.

Akizungumza na wandishi wa habari jijini Dar es Salam jana, wakati wa mkutano wa kujadili uanzishwaji wa mitaala hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa chuo hicho, alisema mafunzo ya wataalamu hao yatakuwa ya ngazi ya shahada ya uzamili.
Alibainisha kuwa mitaala hiyo itajihusisha katika kutoa na mafunzo kwa wataalamu haswa katika sekta ya bandari, reli, barabara, upande viwanja vya ndege na maeneo mengine yanayohusu usafirishaji.
Maganilwa alisema serikali inakabiliwa na uhaba wa wataalamu hao, huku wachache waliopo kuamua kubobea zaidi katika sekta ya viwanda.
Aidha, serikali imeamua kuimarisha miundombinu ya reli baada ya kubaini kuwa ndiyo chachu ya maendeleo hivyo inalazika kukifufua chuo cha watalamu Tabora ambacho walikitelekeza na kutegemea waalamu zaidi kutoka Shirika la Reli la Tanzania na Zambia (TAZARA), ambao nao sasa wamezeeka hivyo kuna ulazima wa chuo chetu kutoa mafunzo ya aina hiyo kwa vijana wenye damu changa.
“Tukubali kuwa nchi inapokuwa na miundombinu ya uhakika ni fursa ambayo inasaidia kuinua uchumi wa nchi hivyo kuanzishwa kwa mafunzo ya wataalamu hao kutakuwa chachu kubwa ya kutuletea mabadiliko katika usafirishaji”alisema Maganilwa.
Maganilwa aliongeza kuwa wataalamu hao ni muhimu katika sekta mbalimbali kwani uwepo wao utasaidia zaidi katika kuliletea taifa hili maendeleo ambayo ndiyo kiu ya jamii.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top