Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

TANZANIA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO WA VIJANA WA KANDA YA AFRIKA YA JUMUIYA YA MADOLA


 

DAR ES SALAAM, Tanzania

TANZANIA inatarajiwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Vijana wa Kanda ya Afrika wa Jumuiya ya Madola kuanzia Januari 28 hadi Februari Mosi, mwakani.

Mkurugenzi wa Kanda ya Afrika ya Mpango wa Vijana wa Jumuia ya Madola, James Odit, aliyasema hayo leo jijini Dar es Salaam, wakati alipokuwa kizungumza na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara kuhusu maandalizi ya mkutano huo.
Mkurugenzi huyo, alisema mkutano huo utahusisha nchi 22 ambazo ni wanachama na jumla ya washiriki 60 wanatarajiwa kuhudhuria mkutano huo kutoka katika wizara zinazohusiana na masuala ya vijana, viogozi wa vijana, viongozi wawakilishi wa Baraza la Vijana, wawakilishi wa kimataifa, viongozi wa kikanda wa maendeleo ya vijana na Jumuiya ya Madola.
Miongoni mwa mambo mengine waliyojadiliana ni utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Vijana na jinsi ya kuunda Katiba ya Baraza la Vijana la Jumuiya ya Madola.
“Mkutano huu utajadili namna ya kuunda Baraza la Vijana la Jumuiya ya Madola (CYC), program za maendeleo ya vijana na jinsi ya kuwawezesha katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo,” alisema Odit.
Kwa Upande wake Waziri wa wizara hiyo, Dk. Mukangara alisema anaishukuru jumuiya hiyo kwa kuichagua Tanzania kuwa mwejeji wa mkutano huo.
Hata hivyo, aliema suala la uundaji wa Baraza la Taifa la Vijana hivi sasa liko katika hatua ya ngazi za juu.
Dk. Mukangara alizitaja baadhi ya changamoto za kuendeleza mipago mbalimbali ya maendedeleo ya vijana kuwa ni pamoja na ukosefu wa fedha za kutosha, mfano kama vile kuwawezesha vijana katika shughuli za kiuchumi na kimaendeleo, kuwajengea uwezo, kuwapatia ajira, ujuzi na elimu.
Waziri Mukangara aliishauri Jumuiya hiyo kuangalia namna ya kushirikiana katika maeneo mengine kama vile sekta ya Michezo, Utamaduni na Habari.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top