Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

TBL YASHINDA RUFAA YA KUTOILIPA SBL

 


KAMPUNI ya Bia Tanzania Breweries Limited (TBL), imeshinda kesi inayohusisha malipo ya Sh25 bilioni dhidi ya Kampuni ya Serengeti Breweries Limited (SBL) katika hukumu iliyotolewa na Baraza la Ushindani nchini (FCT).
Tume ya Ushindani nchini, mwaka 2010 iliitoza faini ya asilimia tano ya mauzo TBL, kwa kujihusisha na tabia kinzani za ushindani wa biashara dhidi ya (SBL), asilimia hiyo inafikia takriban Sh25 bilioni.
Kutokana na uamuzi huo, TBL kupitia mawakili wake ambao ni Dk Ringo Tenga na Fayaz Bhojan walikata rufani.
Katika rufani hiyo, mawakili hao wa TBL waliwasilisha hoja mbalimbali, ikiwamo ya FCC haikuundwa ipasavyo kwa mujibu wa sheria na kwamba mwenyekiti wake, Nikubuka Shimwela hakuteuliwa kama inavyostahili.
Mawakili hao waliendelea kudai kuwa, Mwenyekiti huyo aliteuliwa na Waziri wa Biashara siyo Rais wa nchi kama sheria ya ushindani inavyoelekeza, hivyo kufanya uamuzi uliotolewa kuwa batili na unastahili kufutwa.
Licha ya hoja hizo, mawakili hao wa TBL pia walidai kuwa, Mkurugenzi huyo wa FCC naye hakuteuliwa kihalali.
Jopo la watu watatu, lililoongozwa na Jaji wa Mahakama Kuu, Razia Sheikh lilisikiliza rufani na kukubaliana kuwa FCC kwa kipindi hicho haikuwa imeundwa kwa mujibu wa sheria, hivyo uamuzi wa TBL kutoa faini hiyo haukuwa halali.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top