Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

TYSON AZIDI KUWACHANGANYA WAPENZI WAKE BAADA YA KUKANUSHA UVUMI WA KUJIBADILISHA MAUMBILE

Mike Tyson Mike Tyson speaks onstage during the 'Taking On Tyson' panel at the Animal Planet portion of the 2011 Winter TCA press tour held at the Langham Hotel on January 6, 2011 in Pasadena, California.

NEW YORK, Marekani
Bondia bingwa wa zamani wa dunia, Mike 'Iron' Tyson amekanusha uvumi kwamba amefanyiwa upasuaji wa saa 16 kubadili jinsia yake na kuwa mwanamke aliyejipachika jina la Michelle.

Baadhi ya vyombo mbalimbali vya habari Tanzania na kwingineko barani Afrika 'viliingia mkenge' kwa kuripoti uzushi huo kuhusiana na kubadili jinsia kwa Tyson na pia sura yake.

Chanzo cha taarifa hizo ambazo Tyson ameziita kuwa za kipumbavu ni tovuti iitwayo NewsBiscuit, iliyozichapisha mwishoni mwa Novemba.

Baadaye ikaripotiwa na gazeti la Jumapili la Zimbabwe. Tovuti ya Zambia Watchdog ikaidaka stori hiyo Jumatatu na kudakwa na tovuti ya SpyGhana Jumanne.

"Tumekuwa na wasomaji kutoka Afrika katika siku chache zilizopita kama tulivyotarajia kwa mwezi mzima," John O'Farrell wa tovuti ya NewsBiscuit aliiambia BBC, akiongeza kwamba habari hiyo ilisomwa zaidi ya mara 50,000.

Taarifa iliyodaiwa kutolewa na Iron Mike na kukaririwa na tovuti ya Spy Ghana ilisema: "Mimi bado ni mwanaume na siku zote nimekuwa mwanaume rijali na sijawahi kuwa na nia ya kutaka kuwa mwanamke. Madai hayo siyo tu kwamba ni ya uongo, bali ni upumbavu. Nilikuwapo ukumbini Jumamosi kushuhudia pambano la ngumi kati ya Pacquiao na Marquez na mtu yeyote mwenye akili timamu anaweza kueleza wazi kwamba niliyeonekana sikuwa mwingine bali mwanaume wa shoka."
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top