Yvonne Cherryl ‘Monalisa’ anaamini kuwa anastahili kuendelea kuwa mwigizaji bora wa kike katika tasnia ya filamu Tanzania, huku akiamini si kitu kinachopatikana kirahisi bali ni juhudi zake na kuwa makini kwa kile anachokifanya katika tasnia ya filamu.
Monalisa ni moja kati ya wasanii waasisi wa tasnia ya filamu hivi karibuni alitangazwa kama mwigizaji bora wa kike mwaka 2012 na jarida la Bab kubwa. Awali Monalisa amewahi kushinda tuzo nyingi zikiwemo za ZIFF.
2. Irene Uwoya
Muigizaji huyu mrembo bado ameendelea kuwa kipenzi cha wapenzi wengi wa filamu nchini kwa uwezo wake mkubwa wa kuigiza hasa kama msichana jeuri. Mwaka 2012 ameng’ara kwenye filamu kadhaa zikiwemo Dj Benny, Barmaid, Sister Marry na zingine.
3. Elizabeth Michael
Pamoja na kukabiliwa na kesi ya kuua bila kukusudia kutokana na kifo cha Kanumba mwaka huu. Elizabeth Michael aka Lulu bado ameendelea kung’ara katika filamu zilizotoka mwaka huu ikiwemo ile ya Woman of Principle aliyoigiza na Ray.
4.Wema Sepetu
Pamoja na kutoingia sokoni bado, Wema Sepetu mwaka 2012 alifanikiwa kufanya uzinduzi wa filamu uliotumia fedha nyingi zaidi kwa kumleta msanii mahiri Omotola Jalade kwenye uzinduzi wa Superstar.
Wema ameendelea kuonesha uwezo mkubwa kwenye filamu zingine alizoigiza zikiwemo Red Valentine, White Maria, Tafrani, Sakata, Crazy Tenant, Diary, Lerato na Dj Benny.
Mwaka 2012 alifanikiwa kufika kwenye fainali za Ijumaa Sexiest Girl ambapo mshindi alikuwa Jaqueline Wolper.
5.Jaqueline Wolper
Jacqueline Wolper Massawe mshindi wa Ijumaa Sexiest Girl amekuwa kivutio kikubwa katika filamu kutokana na mvuto wake.
Filamu kama Taxi Driver, After Death,Malipo na Princess zilimng’arisha mwaka huu.
CREDIT KWA VITUKO VYA MTAA
Post a Comment