
Pengine hii inawahusu walio
katika ndoa na ambao bado!Ni zipi hasa lugha za mwili katika mapenzi?! Hapa
nnazungumizia
ishara, milio au sauti fulani ambazo ukisikia au
kuona kutoka kwa mwenza wako inakupasa uchukua hatua stahili kulingana na
mzingira husika. Kwa wale ambao tupo katika ndoa naimani unanafasi nzuri ya
kumsoma mwenza wako na kuweza kugundua anahitaji au anamaanisha nini akiwa
hivyo.
Kuna baadhi ya wanawake huwa hawawezi kuwaambia waume zao kwamba
wanawahitaji kimapenzi, badala yake huweza kujitegesha au kujirahisi mbele zao,
kwani wanajua kuwafanyia hivyo kutaamsha hamu kwa waume zao na hatimaye kuipata
starehe hiyo pamoja. Mume yakupasa uwe unausoma mchezo mapema kwani si wanawake
wote wataweza sema au kujitegesha na ndio maana tunasisitiza isipite
wiki bila kupeana na mwenza wako.
Pia wanawake nawashauri wawe
"wachokozi" kidogo maana kuna
wanaume huwa hawaanzi mashambulizi mpaka washambuliwe, kama hali ipo hivyo basi
mwanamke inabidi ndo uwe mpangaji mashambulizi ya awali.
Mwisho
niwaambie Mke na Mume, kama inavyowapasa kujua sehemu za mihemuko baina yenu,
inawapasa pia muelewe lugha za miili yenu. Miili inaongea bwanaa, ipeni
nafasi!!!
Post a Comment