Kamishna wa Haki za
Binaadamu wa Umoja wa Mataifa Navi Pillay ameitaka Mahakama ya Kimataifa ya
Uhalifu ICC kuchunguza vitendo vya uhalifu wa kivita nchini
Syria.
Pillay ameliomba Baraza la
Usalama la Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani kupeleka rekodi za ukiukaji
wa haki za binadamu kwenye mahakama ya ICC mjini The
Hague.
Barua ya malalamiko na
kuomba uchunguzi ufanywe iliwasilishwa na Switzerland na kuungwa mkono na nchi
58.
Baraza la Usalama lenye
wanachama 15 ndilo pekee lenye mamlaka ya kupeleka malalamiko hayo katika
mahakama ya ICC.
Wakati huohuo, waandishi
wawili wameuawa katika mashambulizi wakiwa kazini nchini
Syria.
Mwandishi wa Kifaransa
alikufa katika eneo la kaskazini mwa mji wa Aleppo na mwingine kutoka kituo cha
Televisheni cha Aljazeera aliuawa katika kitongoji cha Basra al-Harir kwenye
jimbo la Daraa.


Post a Comment