Waziri
wa Habari, Vijana,
Utamaduni na Michezo, Dk Fenella Mukangara akiwakagua wachezaji wa timu ya
Mikocheni Warriors na
wachezaji wa timu ya Kawe
Kombaini wakati wa ufunguzi wa michuano ya Kombe la Meya, Manispaa ya Kinondoni,
Dar es
Salaam mwishoni mwa wiki. Kulia ni Meya
wa Manispaa hiyo,
Yusuph
Mwenda.
Meya
wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda (kushoto) akimwongoza Waziri
wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo,
Dk Fenella Mukangara
(katikati), Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Fortunatus
Fwema na viongozi wengine mara baada ya ukaguzi wa
timu
Meya
wa Manispaa ya Kinondoni,
Yusuph Mwenda akizungumza na vyombo vya habari wakati wa ufunguzi wa michuano
hiyo
Waziri
wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk Fenella Mukangara (kulia)
akibadilishana mawazo na Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda wakati wa
ufunguzi wa michuano ya kombe la Meya Manispaa ya Kinondoni, Dar es Salaam
mwishoni mwa wiki
Mshambuliaji
wa Kawe Kombaini, Hassan Ngonyani (kulia)
akitafuta
mbinu za kumtoka beki Ally Ramadhan
wa Mikocheni Warriors wakati wa mechi ya ufunguzi ya
Kombe
la Meya Manispaa ya Kinondoni, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Kawe
walishinda kwa
magoli 3-1.
Golikipa
wa Kawe Kombaini Simon Adamu akiudaka mpira huku wachezaji wa timu ya Mikochezni
Warriors wakijiandaa kupiga
goli. Kawe ilishinda magoli 3-1.
Waziri
wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk Fenella
Mukangara akihutubia wakati
wa ufunguzi wa michuano hiyo. Kulia kwake ni Meya wa Manispaa ya Kinondoni,
Yusuph Mwenda, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Jordna Rugimbana (kuhoto kwake) na
Naibu Meya wa Manispaa hiyo, Songoro Mnyonge
(kushoto).
Waziri
wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk Fenella
Mukangara akikagua timu wakati
wa ufunguzi wa michuano hiyo. kushoto kwake ni Meya wa Manispaa ya Kinondoni,
Yusuph Mwenda. source full shangwe
on Sunday, January 20, 2013
Post a Comment