Wanachama wa timu ya Yanga 
kutoka sehemu mbalimbali wakitawanyika nje ya jengo la bwalo la Maofisa wa 
Polisi,Oysterbay jijini Dar mapema leo mchana mara baada ya kumalizika mkutano 
wao mkuu wa Mwaka,ambao kwa hakika umefanikiwa kwa kiasi kikubwa,Mkutano huo 
uliratibiwa na kampuni ya Prime Time Promotions Ltd ya jijini Dar na kurushwa 
Live kupitia Clouds TV,aidha Mkutano huo ulionekana kunoga zaidi kufuatia timu 
hiyo ya Yanga kuifumua timu ya Black Leopards ya nchini Afrika kusini  katika 
mechi yao ya kirafiki iliyofanyika hapo jana kwenye Uwanja wa Taifa bao 
3-2.
 Mwenyekiti Mpya wa Club ya 
Yanga Africans,Yusuf Manji akifafanua mambo mbalimbali kwenye mkutano 
huo,uliochanganua mambo mbalimbali zikiwemo changamoto za timu hiyo,maendeleo 
yao mbalimbali ikiwemo samabamba na ujenzi wa kiwanja kikubwa cha mpira maeneo 
ya Jangwani,jijini dar,Sahihisho la katiba yao,masuala mbalimbali ya 
yanayohusiana na wanachama wao,ustawi wa wanachama wao,mikataba baina yao na 
wadhamini wao na mambo mengine mbalimbali.
 Sehemu ya meza kuu ya 
mkutano huo ilivyokuwa.
 Makamu mwenyekiti wa timu 
ya Yanga,Clement Sanga akitolea ufafanuzi moja ya jambo lililoulizwa na wajumbe 
wa mkutano huo.
Pichani kulia ni mchezaji 
wa timu ya Yanga,Shadrack Nsajigwa akipeana mkono wa shukurani na Mwenyekiti wa 
Yanga,Yusuf Manji mara baada ya kutajwa kuwa ndiye mchezaji aliyedumu Yanga kwa 
muda mrefu miongoni mwa wachezaji waliopo hivi sasa,hivyo alizawadiwa barua ya 
shukurani na kitita cha shilingi milioni moja.
Pichani juu na chini ni 
baadhi ya Wajumbe wa timu ya Yanga waliopata nafasi ya kuuliza maswali 
mbalimbali kwa Kamati ya Utendaji,mbele ya wageni waalikwa mbalimbali 
waliohudhuria mkutano huo.
 Mwenyekiti wa Yanga,Yusuf 
Manji sambamba na Makamu mwenyekiti wa timu hiyo,Clement Sanga wakifatilia jambo 
kwa  makini ukumbini humo.
 Pichani baadhi ya 
wachezaji wa timu ya Yanga pia walihudhuria mkutano huo uliohusu mikakati 
mbalimbali ya kuimarisha timu hiyo.
 Baadhi ya Wazee wa baraza 
wa timu ya Yanga wakifautilia kwa makini yaliyokuwa yakijili kwenye mkutano huo 
mkuu wa Kihistoria.
 Kocha mpya wa timu ya 
Yanga,kutoka nchini Uholanzi Ernest Brandts nae aliruhusiwa kutoa yake machache 
kuhusina na timu yake ya Yanga.
 Pichani ni baadhi ya 
Wanachama wa Yanga waliofurika kwa wingi ndani ya mkutano mkuu wa timu hiyo 
uliofanyika ndani ya bwalo la Maofisa wa Polisi,Oysterbay jijini Dar es salaam 
mapema leo asubuhi na kumalizika mapema jioni ya 
leo. 
 Msanii mahiri wa kizazi 
kipya sambamba na wasanii wenzake kutoka THT wakitumbuiza kwenye mkutano 
huo.
Mtangazaji machachari wa 
kipindi cha michezo,Clouds FM/TV Mbwiga Mbwiguke akiwaweka sawa wanachama wa 
Yanga waliojitokeza kwa wingi kwenye mkutano wao mkuu wa 
Mwaka.

















Post a Comment