Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

PROF.MAGHEMBE AKUTANA NA UJUMBE WA WIZARA YA MAJI YA MISRI, MTO NILE,ZIWA VICTORIA VYATAWALA MJADALA


Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof. Jumanne Maghembe (kulia) akizungumza na ujumbe wa watu wa Misri ulioongozwa na Waziri wa Maji wa nchi hiyo Dk.Mohamed Saad (kushoto) walipofika ofisini kwake kwaajili ya mazungumzo mbalimbali kuhusu sekta ya maji na umwagiliaji hassa suala la maji ya mto Nile ambayo chanzo chake ni ziwa Victoria. Magembe aliwataka kuimarisha Ushirikiano wa nchi hizo kwenye mambo yote wanayokubaliana na kwayale wasiokubaliana kuendelea na majadiliano.
Waziri wa Maji wa nchini Misri Dk.Mohamed Saad (katikati) akizungumza kwenye mkutano na Waziri wa maji na Maofisa wa Wizara hiyo jijini Dar es Salaam leo, ambapo ujumbe huo wa Misri upo nchini pamoja na mambo mengine watajadili suala la maji ya Mto Nile ambayo Chanzo chake ni ziwa Victoria.
Baadhi ya wajumbe walioshiriki mkutano huo kwenye Ofisi za Wizara ya Maji na Umwagiliaji jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Maji wa Misri  Mohamed Saad (katikati) akizungumza na watendaji wa Wizara ya Maji nchini kulia ni Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof.Jumanne Maghembe kushoto ni Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mhandisi Bilinith Mahenge.
Wajumbe wa Serikali ya Tanzania wakinukuu mambo mbalimbali yaliyokuwa yakielezwa na ujumbe wa Wizara ya maji ya nchini Misri jijini Dar es Salaam leo.
Balozi wa Misri nchini Tanzania Hossam Moharam (kushoto) akiwa sambamba ujumbe wa nchiyake uliofika nchini kwa majadiliano ya mambo mbalimbali ya sekta ya maji.
Ujumbe wa Wizara ya Maji ya nchini Misri ukifuatilia majadiliano.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top