Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

TANZANIA YAANZA RASMI KUTUMIA MFUMO WA KIMATAIFA WA UKAGUZI


Mohamed-Mtonga
 Tanzania imeanza kutumia rasmi mfumo wa kimataifa katika masuala ya ukaguzi wa ndani ambapomfumo huo utaweza kupunguza Viashiria mbalimbali vya ubadilifu wa fedha za umma
 Hayo yamebinishwa  leo na mkaguzi mkuu wa ndani hapa Nchini Bw Mohamed Mtonga wakati akifungua mafunzo kwa wakaguzi wa ndani kutoka katika kanda ya kaskazini
 Mohamed alisema kuwa mpango huo wa ukaguzi kwa mfumo wa Kimataifa umeanza kutumika rasmi hapa nchini July  Mosi ambapo utaweza kutoa na kuonesha viashiria mbalimbali ambavyo vinakwamisha shuguli za ukaguzi ndani ya Serikali kuu pamoja na  Serikali za Mitaa.
 Alisema kuwa kupitia mfumo huo mpya wa kimataifa wa ukaguzi wa ndani utaweza kuboresha  na kuwafanya wakaguzi wa ndani kufanya kazi zao kwa uhuru zaidi tofauti na mfumo uliokuwa hapo awali ambao ulikua hautoi fursa kwa wakaguzi wa ndani

 Alifafanua kuwa hapo awali wakaguzi wa ndani walikuwa wanashindwa kutekeleza  majukumu yao kutokana na viashiria vya vitu mbalimbali kama vile rushwa na uhusiano baina ya mkaguzi na mkaguliwa hali ambayo ilikuwa chanzo cha kukwamisha malengo mbalimbali ya ukaguzi hapa nchini ingawaje  ndani ya mfumo wa ukaguzi kimataifa suala hilo halipo kabisa.
 “leo tumewakutanisha wakaguzi  wa ndani kutoka kanda hii ya kaskazini lengo likiwa ni kuhakikisha kuwa wanabadilika na wanaanza kwenda na mfumo huu mpya  wa ukaguzi wa Kimataifa ili tuweze kufikia katika malengo mbalimbali ambayo kwa kweli tunayataka sasa ni wajibu wa  kila mkaguzi wa ndani kuhakikisha kuwa anafuata kanuni   hizi za Kimataifa na kama hatafuata basi Sheria itambana”alisema Bw Mohamed
 Katika hatua nyingine alisema kuwa wakaguzi wa ndani bado wanakabiliwa na changamoto ya uhaba wa bajeti hali ambayo nayo inafanya washindwe kufanya kazi na kukagua miradi kwa wakati husika
 Alisema kuwa kwa sasa wakaguzi wa ndani wanashindwa kufika kwenye miradi tena  kwa wakati kutokana na uhaba wa bajeti ambazo zinatengwa na  Halmashauri huku hali hiyo pia ikichangia sana kutofikia malengo mbalimbali ya kiukaguzi ambayo  yanatakiwa kuwekwa na pia  kusaidia jamii
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top