Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Yanga yawakung'uta Black Leopards 3-2 Taifa


 

Kikosi cha Yanga

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

MABINGWA wa zamani wa Tanzania Bara, Yanga SC, leo imewaangushia kipigo cha mbwa mwizi wageni wao, timu ya Black Leopards ya Afrika Kusini, baada ya kuwatandika mabao 3-2.

Mabao ya Yanga yalipatikana katika dakika ya 32 lililowekwa kimiani kwa njia ya penati na Jerryson Tegete, Frank Domayo dakika ya 63, kabla ya 72 Tegete alipoongeza kalamu ya mabao kwa kuandika bao la tatu.

Mabao ya Black Leopards yalipatikana katika dakika ya 46 lililofungwa na Hampherey Khoza, huku lile la pili likifungwa na Rodney Ramagaleki katika dakika ya 88, hivyo matokeo kuwa bao 3-2.

Mchezo huo ulikuwa na ushindani wa aina yake, kutokana na timu zote mbili kukamiana kwa ajili ya kuipatia ushindi, ila Yanga wao walikuwa juu zaidi na kufanikiwa kuibuka na ushindi huo mnono.

Mchezo huo ni wa Kimataifa wa kirafiki uliowakutani katika Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam, ukiwa ni mchezo mahususi kwa ajili ya kuwapima wachezaji wa Jangwani waliokuwa kambi ya wiki mbili nchini Uturuki.

Pia mchezo huo ni sehemu ya maandalizi kwa timu ya Yanga inayojiandaa na mzunguuko wa pili wa Ligi ya Tanzania Bara, huku wao wakiwa kileleni.

PICHA ZAIDI ZA MECHI HIYO .....


Yanga 3-2 Black Leopard


Golikipa wa timu ya Black Leopards,Ayanda Mtshali akijaribu kuokoa mpira uliotinga kimiani kwa njia ya penati na mchezaji wa yanga,Jerson Tegete,penati hiyo ilipatikana katika kipindi cha kwanza,katika kuoenesha Yanga wako fiti mnamo kipindi cha pili mchezaji akaongeza goli la pili,haikutosha Tegete tena akapachika goli la 3.Ihii ndiyo Yangaa.

Mchezaji wa timu ya Yanga,Mbuyu Twite akimtoka mchezaji wa timu ya Black Leopards ya Afrika Kusini.Ama kwa hakika ihiiii ndiyo Yanga ya Uturuki iliotandaza kabumbu safi kabisa ndani ya Uwanja wa Taifa.
Mchezaji wa timu ya Yanga,Frank Domayo akitaka kumtoka mchezaji wa timu ya Black Leopards ya Afrika Kusini,kwenye mchezo wao wa kirafiki unaofanyika kwenye Uwanja wa Taifa hivi sasa.
Baadhi ya mashabiki wakifuatilia mtanange wa Yanga na timu ya Black Leopards ya Afrika Kusini.
Mashabiki wa yanga kibao
Full Nginja ngijaaa

Mashabiki kwa shangwe kila wakati wakiipa hamasa ya ushindi timu yao ya Yanga.
Mchezaji wa timu ya Black Leopards ya Afrika Kusini akitaka kuwapangua wachezaji wa timu ya Yanga,aah iwapi kwa taabu sana kama uonavyo pichani.
Baadhi ya wachezaji wa Black Leopards ya Afrika Kusini wakiwa kwenye benchi lao
Baadhi ya makocha wa yanga na wachezaji wakiwa watulia tulii kwenye benchi lao la Ufundi
Sehemu ya kikosi kazi cha Clouds TV kinachorusha mtanange huo live kupitia Clouds TV jioni ya leo
Wachezaji wa timu ya Yanga wakiingia iwanja kuiana ngwe ya kwanza.
Hiki ndiyo kikosi kazi cha Yanga
Kikosi cha Black Leopards ya Afrika Kusini.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top