Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

SIASA ZA MAKUNDI YA URAIS ZAIVURUGA CCM ARUSHA

Tukio la kusimamishwa kwa mwenyekiti wa wa jumuiya ya umoja wa vijana wa Chama Cha Mapinduzi(Uvccm) wilaya ya Arumeru mkoani Arusha,Boniphace Mungaya limehusishwa na mlengo wa siasa za makundi ndani ya chama hicho tawala.
Mungaya,alisimamishwa ili kupisha uchunguzi mnamo oktoba mwaka jana baada ya kuandikiwa barua na katibu wa CCM mkoani hapa,Mary Chatanda akituhumiwa kuwa ni mlinzi wa mwenyekiti wa Chadema taifa,Freemam Mbowe na mara kwa mara amekuwa akionekana naye.
Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali vya habari vimedai kwamba Mungaya anahusishwa na mtandao wa mbunge wa Monduli,Edward Lowasa ambaye anatajwa kuwa ni miongoni mwa wanachama wa CCM wanaowania mbio za urais mwaka 2015.
Vyanzo hivyo vya habari vimemtaja Chatanda ambaye alimwandikia barua ya kumsimamisha Mungaya kuwa anahusika katika kundi la waziri ya mambo ya nje ya ushirikiano wa kimataifa,Bernad Membe ambaye naye anatajwa kuwa miongoni mwa vigogo wanaopigana vikumbo kuwania urais mwaka 2015.
Hatahivyo,taarifa mbalimbali zimeeleza kuwa kusimamishwa kwa mwenyekiti huyo kulitokana na kuangushwa vibaya kwa aliyekuwa mgombea wa Uvccm wilayani Arumeru ,Lightness Msemo ambaye ametwaja kuungwa mkono na mtandao wa Membe akiwemo Chatanda.
Wachambuzi wa masuala ya kisiasa mkoani Arusha wamesema kwamba siasa za makundi ndani ya chama hicho ndiyo sababu kuu iliyopelekea kusimamishwa kwa Mungaya ambaye kwa sasa anasubiria uamuzi wa halmashauri kuu ya CCM mkoani Arusha ambayo inatajwa kukaa hivi karibuni kumaliza mzizi wa fitina.
“Ngoja tukwambie Mungaya ameponzwa na siasa za makundi ndani ya chama chetu yeye yuko mtandao wa Lowasa na Chatanda alikuwa na chaguo lake ambaye ni Msemo lakini baada ya kuangushwa kwenye uchaguzi wakaamua kumuundia fitina akasimamishwa”walisema baadhi ya makada wa CCM wilayani Arumeru
Hatahivyo,Mungaya alipotafutwa na gazeti hili ili aweze kujibu madai hayo alikataa kuzungumzia chochote huku akisema kuwa kwa sasa anasubiri uamuzi wa halmashauri kuu ya CCM mkoani Arusha ili aweze kujua hatma yake.
Naye,Chatanda alipotafutwa hivi karibuni na mwandishi wa habari hizi alisema kuwa suala hilo liko ndani ya chama na haliwezi kujadiliwa kwenyen vyombo vya habari.
Mwenyekiti wa CCM mkoani Arusha,Onesmo Ole Nangole alipoulizwa alisema kwamba kwa sasa yuko mapumzikoni wilayani Longido kwa matibabu na kuomba aachwe kwanza mpaka pale atakapopata nafuu.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top