Pinda ametoa
kauli hiyo jana mjini Moshi, wakati akizinduwa mradi waUimarishaji wa Miji 18
za Tanzania bara, ulifadhiliwa na benki ya dunia kwa lengo la
kuimarisha uwezo wa kutekeleza majukumu ya Halimashauri na miji ili kutoa
huduma bora kwa wanachi.
Alisema tatizo
kubwa lililopo ndani ya serikali ni kukosena kwa ufuatiliaji makini wa miradi,
hali inayosababisha miradi kukamilika chini ya kiwango, pamoja na dhamani fedha
kutoendana na kazi husika.
Waziri panda
amesema serikali haitakuwa tayari kusikiliza vigezo wala sababu zozote za
kukwamisha kazi ya mradi huo, wala kufumbia macho uzembe au ubadhilifu wa
fedha au vifaa utakaosababisha kazi kukwama au kutekelezwa chini ya kiwango.
Amesema
litakuwa jambo la kusikitisha na kusononesha endapo itatokea mojawapo ya
halimashauri kati ya 18 zilizochaguliwa, kuishia njiani bila kukamilisha mradi
huo kwa muda wa miaka mitano.
Amebainisha
mradi huo utaongeza imani kwa wananchi na kuvutia wadau wengine kushirikiana na
halimashauri za hapa nchini, hivyo wakurugenzi wanatakiwa kuomba ushauri kwa
viongozi pale wanapoona kuna dalili za vikwazo ambavyo vinaweza kusababisha
ucheleweshaji wa utekelezaji wa mradi.
Pinda amesema
njia ya kufikia mafanikio ya mradi huo ni kuwepo kwa uwajibikaji, utunzani wa
miradi iliyokamilika, ukusanyaji wa mapato, pamoja na ushirikishwaji wa
wananchi kwa kushirikisha ngazi zote ikiwa ni pamoja na taarifa za utekelezaji
wa mradi ziwekwe wazi.
Ametaja maeneo
mengine ya mradi utakapolenga kuwa ni uboreshaji wa mifumo ya udhibiti wa fedha
manunuzi ya maswala ya mazingira, mfumo wa utekelezaji utunzaji wa miundombinu
kwa ajili ya huduma za jamii, na kuboresha uwajibikaji.
Mwandishi: Arnold
Swai, Moshi-Kilimanjaro
Post a Comment