Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

LOWASSA AUNGURUMISHA VILIVYO HARAMBEE YA KUCHANGIA UBORESHAJI RADIO IQRA; YAVUKA MALENGO ZAIDI YA MILIONI 590 ZACHANGWA .... HAYA HAPA MATUKIO YOTE YALIYOJILI HATUA KWA HATUA KIUKAMILIFU

Waziri Mkuu mstaafu Mhe. Edward Lowassa akizungumza na wananchi waliojitokeza katika hafla ya Harambee iliyofanyika katika Hotel Gold Crest jijini Mwanza, kuwahamasisha kutambua nini wanapaswa kufanya ili kufanikisha lengo lililokusudiwa. 
Na Albert G. Sengo
MWANZA.
WAZIRI Mkuu mstaafa Mhe.Edward Lowassa ijumaa usiku aliongoza harambee kubwa  na ya kihistoria ya kuchangia kituo cha Redio IQRA Fm kinachomilikiwa na Baraza Kuu la Waislamu Mkoa wa Mwanza (BAKWATA) iliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Gold Crest Jijini Mwanza.

Mhe.Lowassa aliyekuwa Jijini Mwanza kushirikiana na marafiki zake, wafanyabiashara, taasisi na  makampuni mbalimbali, watu binafisi na viongozi wa serikali na vyama vya siasa na wabunge wa majimbo mawili ya jijini Mwanza Ilemela na Nyamagana kupitia CHADEMA yaliyotuma wawakilishi wao hatimaye aliweza kuvuka lengo lililowekwa kwa kukusanya zaidi ya shilingi milioni 590 zikiwemo ahadi.
Mfanyabiashara maarufu jijini Mwanza ambaye pia ni Mzee wa baraza la wazee Mwanza Mjumbe wa NEC wilaya ya Tarime Mhe. Christopher Gachuma akimkabidhi mmoja wa wazee wa kiislamu aliyeketimeza kuu kanzu pamoja na joho kama zawadi aliyovikwa  mgeni rasmi  Mhe. Lowassa.
Lilikuwa tukio la kipekee Mhe. Lowassa alivikwa na kukabidhiwa zawadi ya kibarakashia juu..
Katibu wa BAKWATA  mkoa wa Mwanza Shekhe Mohamed Bala akizungumza na hafla hiyo ya harambee kuchangia maboresho ya radio za kiislamu zenye lengo la kutoa elimu zaidi kwa umma.
"Ninaamini vituo vya redio Iqra FM na redio Sauti ya Qur-ani kitaonyesha Uislamu kama dira unayohusisha mambo yahusuyo jamii. Ni cheche ya kimungu ambayo inatoa ubinafsi pia inayo waunganisha binadamu katika jamii moja. Korani inasema binadamu ameumbwa kutokana na roho moja, kama mwanaume na mwanamke, jamii na mataifa, ili watu waweze kufahamiana. Inawaleta watu wa imani zote kwenye jukwaa moja, kwa kupitia wema."

CHANGIZO LIKAANZA:


























CREDITS:  GSENGO BLOG
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top