Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Ni Mugabe tena,raisi wa Zimbabwe

 


Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe aataendelea na awamu ya saba ya uongozi nchini humo baada ya Tume ya taifa hilo ya uchaguzi kumtangaza mshindi
Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe aataendelea na
awamu ya saba ya uongozi nchini humo baada ya
Tume ya taifa hilo ya uchaguzi kumtangaza mshindi
REUTERS/Philimon Bulawayo
Na Martha Saranga Amini

Hatimaye tume ya taifa ya uchaguzi nchini Zimbabwe imetangaza matokeo ya urais na rais Robert Mugabe kuibuka mshindi kwa asilimia 61.09 akifuatiwa na mpinzani wake waziri mkuu Morgan Tsvangirai,matokeo ambayo yalikuwa yakisubiriwa kwa hamu na ulimwengu mzima.

Awali Waziri mkuu Tsvangirai alilalamikia uchaguzi wa wabunge na uraisi kugubikwa na utata na kuahidi kuchukua hatua za kisheria kupinga matokeo hayo.

Bwana Tsvangirai alidai kuwa chama chake cha MDC hakitakuwa radhi kushirikiana na chama cha raisi Mugabe Zanu-PF.

Vyama hivyo vikuu vya siasa nchini Zimbabwe vimekuwa katika mgogoro tangu mwaka 2009 baada ya uchaguzi mkuu uliopita ambapo uligubikwa na ghasia.

Matokeo ya mwishoni mwa juma yalionesha chama cha MDC kilibananishwa na kupata ushindi hafifu wa viti vya ubunge 49 wakati chama cha raisi Mugabe Zanu-PF kkikijizolea jumla ya viti 158.

Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top