Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

DKT. MAHENGE : Serikali ina dhamana ya kuhakikisha sekta ya maji inapiga hatua kubwa

 


DSC07114
Mhe. NWMA, Dk. Binilith Mahenge akiwa katika chanzo cha maji,  Ng’humbi. DSC07131
Mhe. NWMA, Dk. Binilith Mahenge akiwa katika harakati za kukagua   tanki la mradi wa maji wa Mkoka. DSC07136
Mhe. NWMA, Dk. Binilith Mahenge akisikiliza maelezo akiwa juu ya tanki la kuhifadhi maji, mradi wa maji Ng’humbi. DSC07154
Tenki la kuhifadhi maji, mradi wa maji Kibaigwa.


BRN yampeleka NWMA Dodoma
Mhe. Naibu Waziri wa Maji, Dk. Binilith Mahenge ameendelea na ziara yake mkoani Dodoma kuangalia utekelezaji wa miradi ya maji ya vijiji 10 katika Halmashauri za mkoa huo kupitia mpango wa Big Results Now.
“Serikali ina dhamana ya kuhakikisha sekta ya maji inapiga hatua kubwa na kupitia Wizara ya Maji, itahakikisha vijiji 10 katika Halmashauri zote nchini zinapata maji kufikia Juni, 2015.” alisema Dk. Mahenge.
Dk. Mahenge alisisitiza ni wakati wa viongozi kuanzia ngazi ya Halmashauri kusimamia kwa ufanisi utekelezaji wa miradi hiyo kwa maendeleo ya nchi. Kutokana na wananchi kutumia muda mwingi kutafuta maji baadala ya kufanya shughuli za kila siku za maendeleo kama kilimo na elimu.
Aliagiza ufuatiliaji na usimamizi wa karibu wa utekelezaji wa miradi iliyopangwa, kwani bila hivyo hakutakuwa na mafanikio yoyote. Pia, aliwaasa wananchi kushiriki katika kuchangia fedha kiasi kidogo kwa ajili ya kuhakikisha miradi hiyo ili iwe endelevu na kudumu kwa vizazi vijavyo.
Dk. Mahenge alitembelea pia mradi wa Ntomoko, wilayani Kondoa kujionea utekelezaji wake ambao umekua ukisuasua katika utekelezaji wake.
Ambapo hakuridhishwa na utekelezaji wa mradi huo kwa ujumla, pamoja na kukuta wingi wa maji katika mradi huo, huku miundombinu yake ikiwa hairidhishi.
 
 
Dk. Mahenge aliagiza mapungufu yote ya  mradi huo yafanyiwe kazi na kuhakikisha unatekelezwa kwa haraka, kwani Waziri Mkuu alishatoa karibu Sh. Bil 3 ili ukamilike, na unategemewa kumaliza tatizo la maji wilayani Kondoa na maeneo jirani.
Vilevile, Dk. Mahenge, alifanikiwa kutembelea miradi ya Chunyu, Kimagai, Kidenge, Ng’humbi, Kibaigwa, na Mkoka kujionea maendeleo ya miradi hiyo hadi kufikia sasa na kwa kiasi kikubwa alidhirishwa na hali aliyoiona katika ziara yake hiyo.
Dk. Mahenge yuko mjini Dodoma kwa ziara ya siku 5 kuhakikisha sekta na ametembelea wilaya za Mpwapwa, Kongwa, Kondoa na Chemba na anategemea kumaliza ziara yake leo Jumamosi.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top