Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Elimu ni nyenzo ya kupambana na VVU, dawa za kulevya kwa Vijana – Mama Salma Kikwete

 

IMG_1885
Mama Salma Kikwete akipewa zawadi ya mkanda wa kimasai toka kwa mmoja wa wazee wa kimasai ikiwa kama zawadi kwa Mheshimiwa Rais Kikwete.
IMG_1890
Chifu wa Kimasai Tikwa Morezo (Oloiboni) akizungumza kwa niaba ya wazee wa Kimasai.
IMG_1893
Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia tukio hilo la warsha ya viongozi wa Kimila wa jamii ya wafugaji.
IMG_1855
IMG_1857
IMG_1904
Mgeni Rasmi Mama Salma kikwete akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wageni waalikwa.
.asilimia 40 ya watoto wa kike kukosa fursa ya elimu nchini

Na Damas Makangale, Moblog
Mama Salma kikwete amesema kuwa elimu ni msingi utakaomwezesha kijana kujiepusha na changamoto za aina mbalimbali kama mimba za utotoni, maambukizi ya VVU na dawa za kulevya.
Akizungumza kwenye uzinduzi wa warsha ya viongozi wa Kimila wa jamii ya wafugaji jijini Dar es Salaam, Mama Kikwete amesema elimu inamuwezesha kijana kutumia fursa za maendeleo ya kiuchumi zilizopo hapa nchini.
“kwa bahati mbaya sana kutokana na sababu mbalimbali wasichana wameachwa nyuma sana katika fursa za elimu kuanzia elimu ya sekondari hadi vyuo vikuu,,” amesema
Mama Kikwete alifafanua kwamba kwa kiasi kikubwa katika maeneo ya vijijini ambapo asilimia 40 ya watoto wa kike wanakosa fursa ya kupata elimu ukilinganisha na asilimia 29 ya watoto wa kiume waliokosa fursa ya elimu.
Amesema wasichana zaidi ya 55,000 wamekuwa wakifukuzwa shule kwa sababu mbalimbali ikiwemo ya ujauzito katika kipindi cha muongo mmoja uliopita.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top