Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Msafara wa Dr. Slaa mkoani kigoma wapingwa kwa maandamano makubwa....CHADEMA watoa picha feki kulinda heshima....SOMA ZAIDI


Kwa  mujibu  wa  ratiba  ya  ziara  ya  Dr. Slaa  iliyotolewa  tarehe  3  disemba  ni  kwamba  leo  tarehe  5  Dr. Slaa   anatakiwa  kuwa  Kakonko...
Kakonko ni jina la makao makuu ya Wilaya ya Kakonko katika Mkoa wa Kigoma.
Taarifa  tulizozipata  zinaarifu  kuwa, msafara  huo  umegonga  kisiki  baada  ya  wananchi  kuvizunguka  viwanja  vya  bunge  ambako  mkutano  huo  unafanyika  huku  wakiwa  na  fimbo  na  mawe....
 
Mbali  na  silaha  hizo, wananchi  hao pia   wamesikika wakiimba  pambio  moja  la   "Tunamtaka Zitto wetu"..

Majira  ya  saa  tisa  na  dakika  kadhaa, gari  ya  M4C    yenye  vijana  watatu  ndani  yake  ilionekana   ikiwazunguka  wananchi  hao   huku  ikiwatishia  kuwakamata  endapo  wataleta  fujo  eneo  hilo.
Baadaye  mkutano  huu  unaonekana  kuanza  huku  Dr. Slaa  akiwa  chini  ya  ulinzi  mkali  wa  vijana  15  wa  Redbrigedi  na  polisi  kadhaa   waliojihami....
Baada  ya  mkutano  kuanza  salam  za  Dr. Slaa  zilipokelewa  kwa  matusi  na  sauti  za  kuzomea  zikisikia  kumtaka  Zitto Kabwe  ambapo Slaa  aliwatuliza  kwa  kuwambia  kuwa  atawaeleza  mwishoni  alipo  Zitto Kabwe...
Dakika  kadhaa  baada  ya  mkutano  kuanza, kijana  mmoja  anaonekana  kutiwa  mbaroni  na  vijana  wa  Redbrigedi  kwa  tuhuma  za  kupiga  picha  kwa  kutumia  simu  yake  bila  ridhaa  yao  huku  wakimtaka  aonyeshe  vitambulisho  vyake  kama  kweli  ni  mwandishi  wa  habari...

Kwa  mujibu  wa  mitandao  mingine, uongozi  wa  CHADEMA  majira  ya  saa  tisa  umepingwa  vikali  na  watanzania  wenye  uchu  wa  kujua  hatima  ya  sekeseke  hili  baada  ya  kutundika  picha  mbili  za  mwaka  2010  wakidai  kuwa  ni  za  leo  katika  mkutano  wa  Dr. Slaa.....
Download Our App

1 comments:

1. Watanzania tumeapa kuitokomeza ccm hata kama ccm wataendelea kuhujumu mikutano ya chadema. CCM endeleeni kuvuruga amani katika mikutano ya chadema lakini mjue kwamba Hatuko tayari kuendelea kutawaliwa na Wezi/Walanguzi/Majangili/Majambazi/Wauaji/watesaji/Mafisadi. Maana halisi ya ufisadi ni Wezi/Walanguzi/Majangili/Majambazi/Wauaji/watesaji/Mafisadi hivyo ccm msizani maovu yenu kuyaita ufisadi maana yake hatujui

Reply

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top