Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

RPC Tabora amkingia kifua mtuhumiwa

 

Kamanda wa Polisi  mkoani Tabora, Peter OumaHATMA ya Mkuu wa Kituo cha Polisi Igunga mkoani Tabora, SP Edson Mfuru anayedaiwa kumuachia mtuhumiwa Magata Singu anayetuhumiwa kumpa mimba mwanafunzi wa darasa la sita mwenye umri wa 14 katika Shule ya Msingi Hani Hani, iliyopo Igunga sasa ipo mikononi mwa kikosi cha kupambana na rushwa (TAKUKURU).
Wakati TAKUKURU wakiingilia kati suala hilo, taarifa zaidi zinasema kuwa Kamanda wa Polisi mkoani Tabora, Peter Ouma anafanya jitihada za kumnusuru SP Mfuru asikabiliane na mkono wa sheria.
Hatua ya RPC Ouma kuhusishwa kumuokoa SP Mfuru, inatokana na madai ya kushindwa kuwachukulia hatua askari wanaodaiwa kuchana karatasi iliyoandikwa maelezo ya binti aliyelalamika (RB) pamoja na ile ya mtuhumiwa kukamatwa kwa mara ya kwanza.
Uamuzi wa TAKUKURU umekuja siku chache baada ya Kamanda Ouma kukutana na OCD wa Igunga, Abed Maige pamoja na OCS Mfuru katika kikao cha ndani ambapo maofisa hao wa polisi walimueleza RPC namna siri za polisi zinavyovujishwa, na kumuomba awasaidie kukabiliana na hali hiyo.

Katika kikao hicho cha ndani, inaelezwa kuwa RPC Ouma aliwaeleza wazi kuwa kukithiri kwa rushwa na kudhulumiana ndiyo chanzo cha baadhi ya mambo ya polisi kuvuja hadharani.
Hata hivyo, katika kikao hicho inaelezwa kuwa lilitolewa agizo la kuwahamisha baadhi ya askari waliotuhumiwa kuwa nyuma ya siri za kuachiwa mtuhumiwa Singu.
Jambo jingine lililosababisha TAKUKURU waingilie kati ni pamoja na mtu aliyemwekea dhamana Singu kuendelea kuwa nje huku mtuhumiwa aliyewekewa dhamana akiwa hajulikani alipo.
“Bado hali ni mbaya na sasa TAKUKURU wameshaingilia kati kwa kuanza kumhoji mlalamikaji na pia kutaka kujua sababu za mtuhumiwa kutofikishwa mahakamani,” kilisema chanzo chetu ndani ya Jeshi la Polisi Igunga.
Kwa mujibu wa habari hizo, miongoni mwa watu watakaotoa maelezo mbele ya TAKUKURU ni pamoja na askari aliyemkamata mtuhumiwa na yule aliyeshika faili la kesi kabla ya mtuhumiwa kuachiwa.
Kamanda wa TAKUKURU Wilaya ya Igunga, John Ngunangwa alipoulizwa juu ya kikosi chake kuingilia kati suala hilo, alikiri kulifuatilia huku akikataa kutoa maelezo zaidi kwa ajili ya kukamilisha taratibu za kuwakamata wahusika.
RPC Ouma alipoulizwa hatua zilizochukuliwa na Jeshi la Polisi kwa watuhumiwa, alisema bado wako kwenye uchunguzi.
Alipotakiwa kueleza kama kunahitajika uchunguzi zaidi ya kuanzia katika kitabu cha kumbukumbu ya matukio ya polisi na kufuatilia namba aliyopewa mlalamikaji katika tuhuma hizo, RPC Ouma alisema yupo katika kikao na kukata simu.
Hivi karibuni, gazeti hili liliandika juu ya mtuhumiwa Magata Singu kuachiwa kwa dhamana ya sh mil. 3.4 kutokana na tuhuma za kumpa mimba mwanafunzi wa darasa la sita mwenye umri wa miaka 14.
Ilielezwa kuwa Novemba 9, wazazi wa mtoto huyo walifika katika Kituo cha Polisi Igunga na kufungua mashitaka na kupewa namba ya jalada, RB IG/1430/2013 na kisha mtuhumiwa kukamatwa Novemba 10 na kuachiwa Novemba 11

TANZANIA DAIMA
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top