Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MADIWANI WA HALMASHAURI YA MJI WA KAHAMA WAFANIKIWA KUPUNGUZA GHARAMA ZA MATIBABU KUTOKA SHILINGI 3000 HADI SHILINGI 1000.


HATIMAYE Madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Kahama juzi wa walibadili  kiwango cha shilingi 3,000 walichokuwa wakitozwa wagonjwa katika Hospitali ya Wilaya kabla ya matibabu hati kufikia kiwango cha shilingi 1,000.
Mabaliko hayo yalikuja katika kikao cha cha makisio ya bajeti ya Halamashauri hiyo kwa mwaka 2014/2015 ambapo Diwani wa viti maalumu Aoko Nyangusu alipotaka kujua kwanini wagonjwa wamekuwa wakitozwa kiasi hicho kikubwa cha fedha.
Nyangusu alisema kuwa kiasi cha shilingi 3,000 wanachotozwa wagonjwa ni kikubwa kwani kuna baadhi ya watu hawana fedha hizo ambazo hutolewa kabla ya matibabu na kuongeza kuwa lazima kipunguzwe ili kila mtu aweze kumudu gharama za matibabu katika Hospitali hiyo.
Hata hivyo Diwani huyo Aoko Nyangusu alisema kuwa mbali na kupunguzwa katika Hospitali ya Wilaya pia alipendekeza pia kiwango cha shilingi 1,000 kilichokuwa kikitozwa katika vituo vya Afya na Zahanati kipinguzwe pia hadi kufikia kiwango cha shilingi 500.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kahama Felix Kimaryo alisema kuwa suala hilo limeptishwa katika baraza hilo la Madiwanik na kuongeza kuwa viwango hivyo vya fedha vitapunguzwa ili kila mwananchi aweze kumudu gharama hizo.
Pamoja na Mambo mengine Halmashauri hiyo ya Mji wa Kahama imeweza kupitisha kiwango cha makisio ya bajeti ya Mwaka 2014/2015 ikiwango cha shilingi bilioni 35.09 kwa mwaka huo ikiwa ni ongezeko la asilimia 53.37 tofauti na mwaka 2013 ilipokuwa kiasi cha shilingi bilioni 22.2.
Akisoma makisio katika kikao cha baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo ya Mji Felix  Kimaryo alisema kuwa katika mapato ya ndani wamekisia kiwango cha shilingi bilioni 2.9 huku changamoto kubwa ikiwa ni kujikita katika kuongeza mapato ya ndani.
Aidha Kimaryo alisema kuwa changamoto nyingine ni baadhi ya wafanyabiashara wa mji wa Kahama kukwepa kulipa mapato katika Halmashauri hiyo ikiwa sambamba na kukwepa kujlipa ushuru kama sheria inavyowaangoza katika katika biashara zao wanazozifanya.
Hata hivyo Mkurugenzi huyo alisema kuwa mikakati iliyonayo Halmashauri yake ni pamoja na kuhakikisha kuwa  inaboresha  usimamizi wa ukususanyaji wa vyanzo vya mapato ya ndani  pamoja na kuhamasisha wafanyabiashara kulipa ushuru kwa mujibu wa sheria.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top