Mkazi wa Mwenge jijini Dar es salaam
Philimon Nelson (45) ambaye alikuwa mfanyakazi wa GEPF amekutwa
amefariki akiwa amelala kitandani chumbani kwake, huku mwili wake ukiwa
hauna jeraha lolote.
Kwa mujibu wa jeshi la polisi kanda
maalum ya Dar es salaam taarifa zinasema kuwa sababu za kifo hicho bado
hazijafahamika ingawaje kwa maelezo ya ndugu wa marehemu walidai kuwa
marehemu enzi za uhai wake alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kifafa.
Na kwasasa maiti imehifadhiwa
hospitali ya Mwananyamala kwa uchunguzi huku upelelezi
ukiendelea.
N katika hatua nyingine jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es
salaam limesema kuwa mnamo januari 19,2014 saa nane kamili
mchana maeneo ya Buguruni Kisiwani maarufu kama Msikitini wa
Msufini ilikutwa maiti ya mtu mmoja mwanaume aliyetambulika kwa
jina la Shabani Rajabu , anayekadiliwa kuwa na umri wa kati
ya 35 hadi 40 ambaye ni mfanyabiashara soko dogo la Kariakoo
ikiwa imelala maeneo hayo na huku mwili wake ukiwa hauna
jeraha lolote.
Aidha Jeshi la polisi kanda maalum
ya Dar es salaam limesema kuwa kuhusu tukio hilo kwa
mujibu wa mashuda walidai kuwa mtu huyo alikuwa akitembea na
ghafla alidondoka chini na kufariki dunia .
Jeshi la polisi kanda maalum ya
dar es salaam limeendelea kusema kuwa chanzo chake bado
hakijafahamika na maiti imehifadhiwa hospitali ya Taifa
Muhimbili.
Post a Comment