RPC -Mungi
******
JESHI la polisi mkoani Iringa linamshikilia Eliabu Myogile (17) mkazi wa Gangilonga kwa kosa la kumbaka mtoto wa miaka miwili.
Akizungumza ofisini
kwake leo Kamanda wa polisi mkoa wa Iringa Ramadhani Mungi
alithibitisha kutokea kwa tukio hilo lililotokea tarehe 19 januari mwaka
huu.
Kamanda
Mungi alisema mtuhumiwa huyo alimbaka mtoto wa kike jina limehifadhiwa
na kumsababishia maumivu makali sehemu za siri, chanzo cha tukio hilo la
ubakaji ni tama ya mwili.
Mbali
na tukio hilo la ubakaji Kamanda Mungi alisema wachumaji wa chai
walioajiriwa pamoja na vibarua wa kiwanda cha chai Kilima estate
kilichopo wilaya ya Mufindi mkoani Iringa walifanya mgomo na kuharibu
mali mbalimbali za kiwanda hicho.
Mungi
alisema chanzo cha mgomo huo ni wafanyakazi kulipwa mshahara mdogo
ambao ulipelekea wafanyakazi hao kuiba mifuko ya saruji na mabati
yaliyohifadhiwa stoo, katika tukio hilo hakuna binadamu yeyote
aliyedhuhurika.
Credit: Francis Godwin blogMWANDISHI ,DIANA BISANGAO WA MATUKIO DAIMA.COM, IRINGA
Post a Comment