Taasisi
ya wanawake na maendeleo (WAMA) na Management Development
For Health (MDH) Tanzania kwa kushirikiana na wizara ya afya
na ustawi wa jamii itafanya mkutano wa kitaifa utakaohusu
kutokomeza maambukizi ya virusi vya UKIMWI kutoka kwa mama
kwenda kwa watoto .
Akizungumza
na waandishi wa habari jijini dar es salaam mkurugenzi wa
idara ya uboreshaji afya wa taasisi ya wanawake na maendeleo
(WAMA) Dr Sarah Maongezi alisema kuwa Mkutano huo unataraji
kufanyika kesho januari 21 ,2014 jijini dar es salaam katika
hoteli ya Serena ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa mheshimiwa
Mama Salma Kikwete , mke wa Rais wa jamhuri ya muungano wa
Tanzania na mwenyekiti wa Taasisis ya wanawake na maendeleo
(WAMA)
Aidha
Dr Maongezi ameongeza kuwa mkutano huo utawahusisha wadau
mbalimbali kutoka wizara ya afya na ustawi wa jamii ,
watendaji katika ngazi ya serikali ya mtaa, mashirika yasiyo
ya kiserikali,wadau wa maendeleo,wanaoishi na maambukizi ya WU
na UKIMWI ,wanataaluma,mashirika ya kidini kwa pamoja wote hao
watashiriki ili waweze kutoa uzoefu wao kuhusiana na changamoto
na mikakati muhimu katika kufikia mafanikio ya malengo ya
mpango wa kitaifa.
Pamoja na hayo Dr Maongezi alisema kuwa ujumbe mkuu wa mkutano huo ni
“Kufanya kazi kwa pamoja kufikia lengo la maambukizi sifuri kwa watoto –Timiza wajibu wako”
Naye
mratibu wa huduma ya mama na mtoto Dr Mary Mwanyika Sando
kutoka Management And Development for Health (MDH) alisema kuwa
wamejikita sana katika kuhakikisha watoa huduma za afya
wanatoa huduma kulingana na taratibau na miongozo ya wizara
ya afya, na hivyo wanajitahidi kutoa msaada ili kuhakikisha
wahudumu wa afya wanapata mafunzo ambayo yanaendana na
miongozo ya wizara ya afya.
Vilevile
Dr Mwanyika amesema kuwa Management And Development For
Health (MDH) kwa kushirikiana na (WAMA ) wamelenga
kuhakikisha kweli Tanzania bila Ukimwi,bila maambukizi mapya na
bila vifo vitokanavyo na ukimwi au unyanyapaa inawezekana na
hivyo wamejitahidi kujikita katika mstari wa mbele ili
kuhakikisha kinamama pamoja na familia zao wanapata hizo
huduma.
Taasisi
ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) ilianzishwa mwaka 2006 na
mheshimiwa mama Salma Kikwete , ni taasisi isiyo ya kiserikali
yenye lengo la kuwaendeleza wanawake na wasichana wa kitanzania
hasa waliotoka katika mazingira hatarishi , na moja ya
malengo ya taasisi ya WAMA ni kuongeza fursa za elimu kwa
watoto wa kike.
Mwandishi Kenneth John wa matukiodaima.com Dar es Salaam
|
on Monday, January 20, 2014
Post a Comment