RPC Mungi
Watu
watatu wafariki dunia katika na wengine kumi kujeruhiwa katika matukio
mawili tofauti likiwemo la mtoto Yusta Mkonda (10) mkazi wa kijiji cha
Migoli mkoani Iringa kutumbukia kisimani.
Akizungumza ofisini
kwake leo Kamanda wa polisi mkoani Iringa Ramadhani Mungi alithibitisha
kutokea kwa tukio hilo lililotokea tarehe 17 januari majira ya saa 12
kamili jioni.
Kamanda
Mungi alisema mtoto huyo ambaye ni mwanafunzi wa darasa la pili katika
shule ya msingi Mtera alitumbukia kisimani alipolkuwa akichota maji.
Wakati
huohuo watu wawili wafariki dunia na wengine kumi kujeruhiwa baada ya
gari walilokuwa wamepanda kuacha njia na kupinduka maeneo ya kijiji cha
Ifwagi wilaya ya Mufindi.
Kamanda
Mungi aliwataja marehemu ni Isack Ngozi (25) pamoja na Paul Mbalinga
(23) ambao walikuwa wamepanda gari aina ya isuzu forward lenye namba za
usajili T 478 ABX mali ya O. Mwidani lililokuwa likiendeshwa na dereva
aliyejulikana kwa jina moja la Nuhu.
Mungi
alisema majeruhi kumi waliokuwemo katika gari hilo walilazwa katika
Hospitali ya Mafinga huku dereva wa gari alikimbia mara baada ya ajali.
Post a Comment