Mkuu wa Wilaya ya Muleba, mkoani Kagera, Lembris Kipuyo.
*****
MKUU wa Wilaya (DC) ya Muleba, mkoani
Kagera, Lembris Kipuyo, amedaiwa kutumia vibaya mamlaka yake na
kuwalazimisha polisi kumkamata Diwani wa Kata ya Magatakalutanga,
Geofrey Ezekiel (CCM), kwa madai ya kumtishia maisha na kutaka kummwagia
tindikali.
Habari
kutoka Muleba zilisema kuwa Kipuyo amekuwa akitoa tuhuma mbalimbali
dhidi ya diwani huyo na kufikia hatua ya kumshitaki katika vikao vya CCM
vilivyoketi Januari 5 na 6 mwaka huu.
Kwa
mujibu wa habari hizo, diwani huyo alilazimika kuandika barua kwa
uongozi wa wilaya wa CCM na kumshitaki mkuu huyo wa wilaya.
Chanzo
hicho kilibainisha kuwa kutokana na hatua hiyo Kipuyo alikimbilia
polisi na kudai kuwa diwani amemtishia maisha na kutaka kummwagia
tindikali, jambo lililolilazimu Jeshi la Polisi kumkamata na kumweka
chini ya ulinzi.
“Hivi
ninavyokwambia diwani huyo ameelekea nyumbani kwake na polisi kwa ajili
ya kwenda kufanya upekuzi,” alisema mtoa habari wetu.
Habari
zaidi zinasema kuwa mgogoro huo unatokana na Kipuyo kuingia katika
vikao viwili vya CCM na cha Kamati ya Siasa ya wilaya, akimtuhumu
diwani huyo kuwa ni mla rushwa na amekuwa akitumia nafasi yake ya
uenyekiti kushirikiana na makandarasi kula fedha za miradi.
Chanzo
hicho kilisema kuwa hata katika kikao cha Januari 6 cha Kamati Kuu ya
wilaya bado mkuu wa wilaya hiyo aliendelea kushusha tuhuma hizo huku
diwani huyo akiwa si miongoni mwa wajumbe waliohudhuria kikao.
“Hatua
hiyo ndiyo ilimsababishia diwani huyo kulazimika kuandika barua kwa
uongozi wa wilaya kulalamikia kitendo hicho na Kipuyo alivyobaini hilo
akaamua kumbadilishia tuhuma na kufungua hiyo ya kumwagiwa tindikali na
kutishiwa maisha,” alisema.
Hata
hivyo gazeti hili lililazimika kumtafuta Kipuyo ambaye alipigiwa simu
na kushindwa kupokea, badala yake alituma ujumbe mfupi wa simu ya
mkononi na kudai kuwa yupo kikaoni, huku akitaka kujua aliyempigia simu.
Akithibitisha
kukamatwa kwa diwani huyo, mmoja wa askari wa jeshi hilo (jina
limehifadhiwa) kwa kuwa si msemaji wa jeshi hilo, alikiri kukamatwa kwa
diwani huyo na kuwa bado wanamshikilia kwa ajili ya uchunguzi wa tukio
hilo.
CHANZO NI TANZANIA DAIMA
Post a Comment